Wednesday, March 26, 2014
KENYATTA ATAJA CHANGAMOTO EAC.
Do you like this story?
Rais uhuru Kenyatta wa
Kenya amesema moja ya changamoto
zinazoikbaili jumuiya ya Afrika
Mashariki (EAC) ni uchumi duni miongoni mwa nchi wananchama.
Akihutubia bunge la
Eela jijini Arusha jana Rais Kenyatta ambaye
ni mwenyekiti wa wakuu wa EAC amesema
ili kujikwamua nchi za kiafrika lazima zijiendeleze kwenye mapinduzi ya viwanda na kujijengea uwezo wa kuongeza thamani bidaa zake badala ya kusafirisha nje malighafi.
Kuongeza thamni bidhaa zetu kabla ya kuzisafirisha licha ya
kukuza uchumi w etu lakini pia
kutaongeza fursa za ajira kwa vijana tofauti na sasa ambapo ajira hizo hupelekwa nje amesema Kenyatta.
Amesema jambo la msingi
katika mapinduzi ya kiuchumi ni umoja na
ushirikiano miongoni mwa wananchi wa EAC
na Afrika kwa ujumla na kutaka viongozi
waliokabidhiwa dhamana kuongoza kwa vitendo
badala ya maneno.
Changamoto zingine
zinazopaswa kushughulikiwa kwa ajili ya ustawi wa umma wa EAC kwa mujibu wa Rais Kenyatta ni vikwazo
vya kibiashara na usafiri miongoni
mwa nchi wanachama.
Amesema nchi za EAC hazina
budi kukabiliana na kupunguza gharama za biashara kulingana na mikataba ya
ushuru wa forodha.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KENYATTA ATAJA CHANGAMOTO EAC.”
Post a Comment