Wednesday, March 26, 2014
WARIOBA AFUNGUKA.
Do you like this story?
Wakati Ikulu ikitangaza kwamba Rais kikwete amevunja tume ya mabadiliko ya katiba, tume hiyo imetoa ufafanuzi wa baadhi ya
maneno ya rasimu ya katiba.
Taarifa ya ikulu
iliyotolewa jana ilieleza kuwa tume ya jaji joseph warioba ilivunjwa tangu
machi 19 ikiwa ni siku moja baada ya kuwasilisha rasimu ya katiba bungeni mjini Dodoma.
Wakati taarifa ya tume ya
warioba ilitolewa jana jioni kurugenzi ya mawasiliano ya Rais , Ikulu ili
kuwa imetosa taarifa ya kuvunja tume
hiyo mapema jana ikileza kuwa shughuli za tume hiyo zilikoma tangu
jumatano iliyopita.
Kwa mujibu wa kifungu cha
31 cha sheria ya mabadiliko ya katiba Rais wa jamhuri ya muungano alivunja rasmi tume ya mabadiliko ya katiba
tarehe 19 machi 2014 kwa tangazo la
serikali na.81 la tarehe 21 machi 2014
ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.
Hata hivyo jaji warioba amesema
jana kuwa hadi wanakutana juzi kwenye
kikao cha mwisho tathmini walikuwa hawajapokea barua ya kuvunjwa kwa tume yake.
Barua ya Ikulu tumeipokea
leo. Tulukuwa hatuna taarifa kwamba tume
yetu imevunjwa hadi tulipopokea
barua leo (Jana) tulifanya kikao chetu
cha mwisho cha tathimini jana (juzi) alisema warioba alipozungumza na mwananchi
jana jioni.
Warioba pia alithibitisha
kwamba tarifa ya ufafanuzi (imechapishwa ukurasa 37) ni ya tume ya mabadiliko
ya katiba.
Taarifa hiyo ya tume ya
warioba imetaja baadhi ya sababu za kupendekezwa kwa muundo wa serikali tatu
kuwa ni pamoja na serikali ya muugano
kutokuwa tena na nguvu upande wa
Zanzibar na Rais kupokwa baadhi ya madaraka aliyopewa kikatiba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WARIOBA AFUNGUKA.”
Post a Comment