Wednesday, March 26, 2014
RAIS AVUNJA TUME YA KATIBA.
Do you like this story?
Rais Jakaya Kikwete
amevunja rasmi tume ya mabadiliko ya katiba
badala ya tume hiyo kumaliza kazi
iliyopewa na kukabidhi rasimu ya katiba kwa bunge maalumu.
Kwa mujibu taarifa kutoka
kurugenzi ya mawasiliano ikulu Rais aliunda tume hiyo kwa muibu wa kifungu cha 5
na cha 6 cha sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya 83
kwa tangazo la serikali na. 110 la mwaka 2012.
Makukumu ya tume hiyo
yalikuwa ni ya pamoja na kukusanya maoni kwa wananchi na kuandaa rasimu ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kazi ambayo imefanywa na tayari imeshwawalishwa kwenye bunge maalumu la katiba.
Tarifa hiyo ilisema kwa
mujibu wa kifungu cha 31 cha sheria ya
mabadiliko ya katiba sura ya 3 Rais alipewa mamlaka ya kuvunja tume ya mabadiliko
ya katiba baada ya rasimu ya katiba
kuwasilishwa bungeni.
Na kwamba mchi 18 mwaka
huu mwenyekiti wat ume hiyo jaji joseph
warioba aliwasilisha rasimu ya katiba
kwenye bunge maalum. Hivyo kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha sheria ya mabadiliko ya katiba rais
alivunja rasmi tume hiyo machi 19 mwaka huu kwa tangazo la serikali
namba 81 la machi 21, 2014.
Hivyo kwa tangazo hilo shughuli zote za tume ya mabadiliko
ya katiba zimemalizika rasmi
tarehe 19 machi 2014.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RAIS AVUNJA TUME YA KATIBA.”
Post a Comment