Monday, March 31, 2014
LOWASSA: HAKUNA KAMA EDWARD SOKOINE.
Do you like this story?
Waziri mkuu mstaafu Edward
lowassa amesema viatu vya hayati waziri mkuu wa tatu Edward sokoine ni bikubwa sana kwamba havivaliki.
Lowassa aliyasema hayo
katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika nyumbani kwake mjini Dodoma
jana.
Mkutano ulisitishwa na mtoto wa hayati sokoine namelok kwa
ajiliya mazungumzo maadhiisho ya miaka
30 tangu kifo cha baba yake, kilichotokana na ajali ya gari dakawa mkoani morogoro.
Havivaliki vile viatu ni
vikubwa sana tumejitahidi kadri ya uwezo wetu lakini marehemu alisema
kumtimikia binadamu ni heshima alisema
wkati akijibu swali aliloulizwa
yeyey kama mbunge wa monduli anadhani ni kwa kiwango gani anaweza kuvaa
viatu vya sokoine.
Amesema eneo ambalo aliliamini snaa hayati sokoini ni
kujenga shule za wasichana hasa kwa
wafugaji.
Amesema kwa kushirikiana
na askofu denis wa kanisa katoliki nchini walitenga eneo monduli juu kwa ajili
ya ujenzi wa shule ya wasichana ya nyakazangai ambayo tayari imeshajengwa.
Aliseme pia wamejenga shule mbili ambapo moja ilijengwa
na kanisa la kiingili la kilutherani
(KKKT) na nyingine imejengwa kwa
utaratibu wa shule za kata.
Aliamini mifugo
lazima iwe na maeneo mazuri na alitenga
maeneo kwa ajili ya wakulima na wafugaji
eneo ambalo wameheshimu sana utaratibu
huu ( wa kutenga maeneo) ni
monduli pale mambo yanakwenda vizuri
alisema.
Alimshukuru raisi kikwte
aliyewasaidia sana wafugaji kwa kuwapatia sh 3 milioni kwa ajili ya ukarabati wa mabawa yaliyopasuka kutokana
na mvua kubwa mwaka juzi ahuku akiongeza kuwa
walipata shida ya njaa kubwa na
kupotea kwa mifugo mingi lakinirais kikwete aliwapatia mifugo 604 ambayo nayo
iliwasaidia sana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “LOWASSA: HAKUNA KAMA EDWARD SOKOINE.”
Post a Comment