Monday, March 31, 2014
MWANGUNGA : PILIPILI USIYOILA YAKUWASHIA NINI?
Do you like this story?
Waziri wa zamani wa maliasili na utalii shamsa mwangunga
amewapiga kijenge wabunge wengine akisema pilipili uliyokula inakuwashia nini?
Mwangunga alizungumzia
sakata la kupiga kura ya siri au ya wazi alisema labda niseme kwa kifupi
sana kwa sabab u sina mengi ya
kuzungumza nimalizie kwa kusema kuwa
pilipili uliyoila yakuwashia nini?
Mjumbe huyo alisema kuwa wanaotaka
kura za siri ni wanafiki kwani wanaficha nini kwa watu ambao waliwatuma kuingia
bungeni humo.
Amesema kuwa kipenda roho
ni kwa mtu kula nyama mbichi hivyo pendekezo la wajumbe kupiga kura za
wazi au ya siri ni pendekezo zuri ambalo linapaswa kuungwa mkono na kila mtu.
Kwa mujibu wa mjumbe huyo
suala la kulazimisha baadhi ya watu
kuingia katika mfumo wa kupiga kura ya siri ni dalili za woga usio na mantiki katika karne ya sasa.
Naye masoud abdalah salim
alizungumzia uamuzi wa kupiga kura mseto
akisema itakuwa ni kioja kupiga kura za aina mbili katika uamuzi wa jambo
moja.
Salim alipendekeza
kuwa kura ya siri ndiyo inayowafikisha
watu mahali ambapo ni salama.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MWANGUNGA : PILIPILI USIYOILA YAKUWASHIA NINI?”
Post a Comment