Monday, March 31, 2014
TMA YAONYA UWAPO WA KIMBUNGA, MVUA.
Do you like this story?
mamlaka ya
hali ya hewa TMAA imetahadharisha
juu ya kuwapo kwa kimbunga kitwacho
chellen katika mwambao wa bahari
ya hindi ambacho kitasababisha mvua
kubwa inayozidi mililita 50 ndani
ya masaa 24 kuanzia jana katika mikoa
24.
Taarif aya mamalaka hiyo
ambayo imetolewa jana kwa vyombo vya habari imebainisha kuwa mvua zitanyesha katika mikoa ya dare s salaam,
mtwara, lindi, tanga,unguja, pemba, singida, Dodoma, Ruvuma, katavi, njombe,
mbeya na morogoro.
Taarifa hiyo imeongeza
kuwa mvua hiyo itarajia kuanza jana zitaendelea hadi april mosi mwaka huu na
wakazi wa mkoa hiyo watuamiaji wa bahari
pamoja na mamlaka zinazohusika na maafa zimetakiwa kuchukua tahadhali zinazotakiwa.
Imebainisha kuwa uwezo wa
mvua hiyo ni asilimia 80 na mwendelezo
wa mvua za masika zinazoendelea kunyesha
nchi nzima katika baadhi ya maeneo ambako hupata misimu miwili ya mvua kwa mwaka.
Mamlaka ya hali ya hewa inaendelea
kufuatilia na itatoa taarifa zaidi kadri zitakavyopatikana alisema sehemu ya
taarifa hiyo na kuongeza kuwa uangalifu
na tahadhari vinahitajika ili kuepusha maafa zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “TMA YAONYA UWAPO WA KIMBUNGA, MVUA.”
Post a Comment