Monday, March 31, 2014

BUNGE LA KATIBA KUANZA KAZI RASMI LEO.





Wakati bunge la katiba leo linaanza  kujadili sura mbili za rasimu  ya katiba ambazo zitalenga  muundo wa muungano, umoja wa katiba  wa wananchi (ukawa)  umewataka wajumbe wake kutokuondoka Dodoma  hadi kumaliza kujadili sura hizo.

Kwa mujibu wa ratiba  ya bunge iliyotangazwa  ijumaa  iliyopita na makamu wenyekiti wa bunge hilo, samia saluhu leo wajumbe watanza kujadili sura ya kwanza  ya rasimu  ambayo inahusu jina mipaka, alama lugha na tunu za taifa.

Sura ya sita inahusu muundo wa muungano  vyombo vya utendaji  na mamlaka ya serikali nchi washirika  na uhusiano wan chi washirika.

Katika bunge la katiba yahaya hamis hamad alisema utaratibu wa kujadili rasimu kwa kuanza na sura hizo umetolewa  na kamati ya uongozi kwa kuaingatia kanuni 58 ya bunge la katiba.

Kanuni hiyo ya 58 inasema kamati ya uongozi itakuwa na majujumu ambayo ni (a) kujadili na kuamua mambo yote yanayohusu uendeshaji  bora wa shughuli za bunge maalumu na kamti zake. B kujadili na kupanga ratiba ya utekelezaji  wa shughuli za bunge na ( c ) kujadili na kufanya uamuzi kuhusu masuala yanayohitaji usuluhishi na maridhiano.


Mjumbe wa bunge  hilo john mnyika  akizungumza kwa niaba  ya mwenyekiti  wa ukawa freeman mbowe  alisema kaunzia leo bunge litaanza kujadili  muundo wa muungano ambao  alisema ndiyo moyo ya rasimu ya katiba hivyo wajumbe wote wa ukawa watashiriki.

Tumewaomba wajumbe kutokuondoka wakati wa kujadili sura hizi mbili kwani ndiyo roho ya rasimu na tunaonya ikifika hatua CCM wakachakachua tutachukua maamuzi  mazito na gharama zozote  alisema mnyika.

Mnyika alisema tayari wamepata taarifa  kuwa wajumbe kutoka CCM wataingia na mapendekezo  yao na yatapigiwa kura kwa kujua wao wapo wengi  pamoja na uteuzi wa wajumbe 201  walioteuliwa na rais jakamya kikwete.

Hata hivyo alisema wakati wa kupitisha vifungu vya rasimu hiyo ni wazi kuwa CCM hain a theluthi mbili kwa Zanzibar  na kama wakipeleka  mapendekezo  ya kutaka kuvunja sheria  na kanuni kwa masilahi yao hawatakubali.

Myika amesema licha ya mwenyekiti  wa kamati ya mabadiliko ya katiba jaji  joseph warioba kueleza upungufu  wa mfumo wa serikali mbili na hivyo kupendekeza serikali tatu ambyo ni maoi ya wnanchi bado CCM inashinikiza na kutetea msimamo wao.


0 Responses to “BUNGE LA KATIBA KUANZA KAZI RASMI LEO.”

Post a Comment

More to Read