Tuesday, March 25, 2014
MAHAKAMA: MTUHUMIWA KESI YA TWIGA AKAMATWE.
Do you like this story?
Mahakama imetoa amri ya
kukamatwa ahmed ambaye ni mshtakiwa namba moja katika kesi ya utoroshaji wa
twiga wane kwenda uarabuni.
Hati ya kukamatwa mshatikiwa huyo ilitolewa jana na hakimu mkazi mfawidhi wa mkoa Kilimanjaro, simon kobelo baada ya mshtakiwa
kushindwa kufika mahakamani jana bila
kutoa sababu.
Amri hiyo inafuatia ombi lililotolewa na wakili wa serikali
evetha muchi baada ya mshtakiwa huyo
kutofika mahakamani kwa siku ya pili mfululizo.
Wakili huyo aliomba
mahakama itoe amri hiyo ili mtuhumiwa
akamatwe na kufikishwa mahakamani leo na kama alikuwa ni mgonjwa awasilishe vyeti kuthibitisha
ugonjwa wake.
Evetha alisema kitendo cha
ahmed kutofika mahakamani bila kutoa sababu zozote kimeisababisha serikali hasara kutokana
na na mawakili hao kusafiri kutoka dare
s salaam hadi moshi.
Hakimu kobelo alikubaliana
na ombi hilo la upande wa mashtaka na kuamuru
mshtatikiwa kukamatwa.
Mwenzi uliopita kesi hiyo
ililazimika kuahirishwa baada ya mshatikiwa
kuugua ghafla muda mfupi kabla ya kesi hiyo inayowakabili pia watanzania
watatu kuanza kusikilizwa.
Watuhumiwa wengine ni hawa mang’unyuka, martin kimath na Michael
mrutu ambao wote wako nje k kwa dhamana .
Wanyama waliotoroshwa walikuwa na thamani y ash 170.5 milioni na
walisafirishwa kwa ndege kubwa ya jeshi
la Qatar.
Ushahidi wa awali mahakamani h apo unaonyesha kuwa
wanyama hao walikamatwa katika maeneo yam to wa mbu. Elboreti na engaruka wilayani monduli.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MAHAKAMA: MTUHUMIWA KESI YA TWIGA AKAMATWE.”
Post a Comment