Monday, March 24, 2014
MBUNGE WA CCM AWEKWA MAHABUSU.
Do you like this story?
Jeshi la polisi wilayani
nzega mkoani hapo limemkamata
mbunge wa jimbo la nzega (CCM) DK
hamis kigwangala kwa kudaiwa kuhamisha
maandamano ya wachimbaji wadogo wa dhahabu
kupinga kufungwa kwa machimbo ya mwashina yaliyo jirani na mgodi wa resolute Tanzania limited.
Kabla ya hapo mbunge huyo
alidaiwa kufanya mkutano mkubwa wa
hadhara na wachimbaji hao katika kijiji
cha nzega ndogo wilayani hapa na alielezwa matatizo ya kufungwa kwa machimbo hayo na kamishana wa madini nchini Paulo Masanja
bila kujali gharama walizoingia wachimbaji hao kwenye eneo hilo.
Katika mkutano huo
wachimbaji hao walidai ni vyema serikali iangalie haki zao katika uendeshaji na
uchimbaji wa mashimo hayo kuliko kuwafungia bila kujali ingawa eneo hilo liko
ndani ya leseni ya mgodi wa resolute lakini wao ndiyo wamiliki wa ardhi
hiyo.
Wachimbaji hao walimwomba
mbunge huyo kuambatana nao kwenye
maandamano ya amani kutoka kijiji cha
nzega ndogo kwenda mwashina yalipo
machimbo yaliyofukiwa, umbali wa zaidi ya kilomita tatu ili kujionea halihalisi
ya kufukiwa kwa eneo hilo na ikiwezekana kufanya mkutano
mwingine wa hadhara kijijini hapo.
Kufuatilia hali hiyo wachimbaji hao walianza maandamano
ambayo yaliungwa mkono na mbunge
huyo hadi kijiji cha mkwajuni kabla ya
kufika mwashina polisi waliiba na kuyasambaratisha maandamano
hayo kwa mabomu ya machozi na risasi
za moto.
Katika na purukushani hizo polisi walimkamata mbunge huyo na kumjeruhi mtu mmoja kwa risasi kwenye paji la uso na
kuondoka naye pamoja na mbunge huyo.
Kamanda wa polisi mkoani
tabora susan kaganda amesema hana taarifa yoyote.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MBUNGE WA CCM AWEKWA MAHABUSU.”
Post a Comment