Monday, March 24, 2014
SULUHU AMEKEA UTORO.
Do you like this story?
Makamu mwenyekiti wa bunge
la katiba, samia suluhu amewataka wajumbe wa bunge hilo kujitahidi kuhudhuria
vikao vya chombo hicho kuwa ndiyo kazi iliyowaleta mjini hapa.
Suluhu amesema hayo muda
mfupo kabla ya kuahirisha semina ya
kanuni za uendeshaji kwa wabunge hao.
“Tumekuja kwa kazi hii ( ya mchakato wa katiba) kwa hiyo waheshimiwa wajumbe wajitahidi kuwepo ndani ya bunge kwa wakati alisema.
Mwananchi alishuhudia viti vingi vya bunge hilo lenye wabunge 629 vikiwa tupu baada ya wabunge wengi kutoingia ndani ya ukumbu huo jioni ama kuinga na kutoka
kabla bunge hilo halijaairishwa.
Kwa mujibu wa katiba
iliyotangazwa asubuhi juzi na mwenyekiti
wa bunge hilo Samuel sitta semina hiyo ilitakiwa kumalizika saa 2: oo usiku.
Tatizo kama hilo la utoro
limekuwa likikemewa mara nyingi na spika wa bunge la jamuhuri ya muungano anne makinda.
Mara kadhaa tatizo hilo limekuwa likisababisha kukwama kwa
maamuzi muhimu yanayohitaji kuamuliwa na wabunge hao.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SULUHU AMEKEA UTORO.”
Post a Comment