Monday, March 24, 2014

IKULU: KUJADILI HOTUBA YA JK KUPOTEZA MUDA.




Mkurugenzi wa mawasiliano  ya Rais I kulu  salva  rweyemamu  amesema kuendela kujadili hotuba  ya Rais  Jakaya Kikwete  aliyotoa kwenye bunge hilo la katiba mwisho  mwa wiki ni kupoteza muda.

Akizungumza jana rweyemamu aliushangaa umoja wa katiba ya wananchi (ukawa)  kuendela kutoa matamko yanayopinga  hotuba hiyo, akisema  haumtendea haki mkuu huyo wan chi na watanzania wote kwa ujumla amesema kama mtanzania Rais  alitoa maoni yake na amekuwa muungwana  kwa kuwambia  kwamba bado  wana fursa ya kujadili na kuleta  mapendekezo  yao lakini wajali zaidi maslahi ya taifa.

Hiyo  ni propaganda  isiyokuwa na maanda kwa taifa na hata  hatima ya katiba yenyewe. Ningependa kuwakumbusha kwamba watanzania wamewapeleka Dodoma  wakajadili  katiba siyo kufanya propaganda tunawataka wakafanye kazi alisema rweyemamu.

Kwa mujibu wa rweyemamu  umoja huo wenye viongozi  kutoka vyama vya  upinzani  haumtendei  haki Rais kwani kama mtanzania  mkuu huyo wan chi ana fursa ya kutoa maoni yake.

“wasifikiri kwa kujibu hivyo Rais wanajibizana na CCM. Rais ni mkuu wan chi ana maoni yake lakini zaidi ya yote, bunge la katiba siyo mahali pa  kufanya siasa kama wanataka  siasa  tunawaomba warudi maofisini  mwao wakafanye  siasa, pale  tumewatuma kazi alisisitiza.

Rweyemamu alibainisha kuwa mchakato wa kutunga katiba  unahitaji busara na hiyo haiwezi kupatikana kama watu wanatumwa kuwawakilisha  wananchi wameamua kufanya siasa.

0 Responses to “IKULU: KUJADILI HOTUBA YA JK KUPOTEZA MUDA.”

Post a Comment

More to Read