Thursday, March 27, 2014
SERIKALI YATOA AMRI YA PIGA "RISASI HADI UUE"
Do you like this story?
SERIKALI
imewaamrisha maafisa wa polisi kuwapiga risasi na kuwauwa washukiwa wa ujambazi
waliowamiminia risasi waumini waliokuwa kanisani siku ya Jumapili na kuwauwa
watu sita huku wengine 17 wakiachwa na mejeraha ya risasi.
Wakati
huo huo polisi wametakiwa kuwauwa majambazi wanaoendelea kuhangaisha wakazi wa
kaunti ya Mombasa.
Akitoa
amri hiyo mwneyekiti wa kamati ya usalama katika kaunti ya Mombasa Bw Nelson
Marwa alisema majangili na magaidi hawafai msamaha, huruma ama kupelekwa
mahakamani huku akivitaka vyombo vya usalama kukabiliana nao mara moja.
Akiongea
kwneye mkutano wa kiusalama kati ya viongozi wa makanisa yote katika kaunti
hiyo kamishna huyu wa kaunti ya Mombasa alisema wahalifu waliouwa wamunimi
kanisani hawafai kupelekwa mahakamani kwa kuua.
“Hao
si watu wakutiwa mbaroni ati kwa sababu wamejihami! Wanafaa kumalizwa papo
hapo. Kwa nini wapelekwe mahakamani ilhali wameuwa watu sita? Kuna haki gani
kwa waliouwawa? Nani atakuwa shahidi yako kortini? Nani atawafufua uliowauwa
ili wawe mashahidi wako? Lazima tuwe watu wa haki wakipatikana wauliwe
maramoja” akaagiza.
Alisema
operesheni ya kuwasaka wahalifu hao imesambazwa hadi kaunti za KIlifi na Kwale
huku akionywa kwamba wataingia hadi katika Kaya kuwasaka.
Alisema
kwa sasa wamekamata washukiwa 109 ambao wamo mikononi mwa maafisa wa polisi
huku akiongeza kuwa hata kivukio cha feri kimezungukwa na maafisa wa polisi
wenye mavazi ya sare na wale wenye mavazi ya kawaida.
“Kivukio
cha Feri inayotumiwa na maelfu ya Wakenya huko tumetuma maafisa wa polisi
washike doria. Wahalifu ambao wametorokea katika Kaya wajue tutawafuata hadi
huko ndani serikali itafanya kile liwezavyo ili wachukuliwe hatua” akasema.
Mwenyekiti
wa muungano wa makanisa Mombasa Askofu Wilred Lai alisema, “Wale ambao
wanadhania watatutishia Kanisani wajue hilo ni ndoto Mkristo hawezi kutishika
na kushindwa kwenda Kanisani. Tutaendelea kuhubiri amani na neon la Munguna
atapambana na nyinyi.”
Walisema
watawasaidia familia za wendazake na walioathirika kwa shambulizi la Kanisani
ikiwemo mazishi.
Bw
Marwa alisema viongozi wa makanisa na misitiki wataunda kamati ambao
itashughulikia maswala ya usalama.
Haya
yanajiri siku moja tu baada ya serikali ya Marekani kuapa kuisaidia nchi ya
Kenya katika kukabiliana na kupambana na ugaidi hususan katika kudhibiti mipaka
ya Kenya.
Maisha
Balozi
wa Marekani humu nchini Robert Godec alisema mashambulizi yanayotekelezwa na
kundi la kigaidi ya Al Shabaab yatahujumu maisha ya wakenya.
“Tunawapa
pole wale wote waliopoteza jamaa zao katika shambulizi la Kanisa. Serikali ya
Marekani inashtumu shambulizi hilo. Serikali ya Marekani itawaunga mkono jeshi
la Kenya (KDF) ipambane na misimamo mikali wanaotekeleza mashambulizi wanafaa
kukamatwa na kushtakiwa” akasema.
Naye
Gavana wa Mombasa Hassan Joho akawarai wakazi wa eneo hilo kusimama pamoja na
kutotikishwa na shambulizi hilo huku akiapa kwamba lililofanyika halitafanyika
tena.
“Hakuna
mtu mwenye ruhusa yakuchukua maisha ya mwenzake hususan mtoto mdogo ambaye hana
hatia alienda kanisani kuomba tu” akasema.
Akiongeza,”
Tunataka waliotekeleza shambulizi hilo wachukuliwe hatua hatutaki watu kupiga
domo tu, uchunguzi w akina ufanywe na haki itendeke.”
Akisisitiza
kwamba, pigana na nafsi yako! acha uhalifu, acha ulevi, swali, fanya ibada
hiyo ndiyo Jihad. Lakini hii kuleta watoto wadogowadogo kuwafundisha uhalifu
kuwatia moto waende wapigane na wengine ati jihad? hakuna Jihad sasa, hakuna,
Jihad iliisha, Jihad iliyobaki ni Jihad yako na Mungu wako wewe kama
binadamu”.
Walikuwa
wakiongea kwenye halfa la kifua kikuu kaunti ya Mombasa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YATOA AMRI YA PIGA "RISASI HADI UUE"”
Post a Comment