Saturday, March 22, 2014
VURUGU ZATOKEA SHINYANGA,NAIBU WAZIRI WA MADINI STEPHEN MASELE APIGWA MABOMU WAKATI WA MCHEZO KATI YA STAND UNITED NA POLISI MARA.
Do you like this story?
Katika
hali isiyo ya kawaida jioni hii kumetokea vurugu katika uwanja wa CCM Kambarage
mjini Shinyanga wakati wa mchezo kati ya Timu ya Stand United ya Shinyanga na
Polisi ya mkoani Mara ambapo wenyeji wa mchezo huo Stand United waliibuka
washindi kwa bao moja dhidi ya Polisi.
Walioshuhudia tukio hilo wamesema vurugu hizo zimetokea mara baada ya machezo
kuisha,ambapo wachezaji wa timu ya Polisi Mara walipotoka uwanjani walimfuata
refa wa mchezo huo pamoja na wasaidizi wake kutaka kumpa kichapo,na kufuatia
hali hiyo baadhi ya watu waliokuwa katika eneo hilo wakiwemo wachezaji wa timu
ya Stand united waliingia uwanjani kutaka kumsaidia refa ili asipigwe.
Kati ya watu walioingia uwanjani hapo,aliyekuwa mbele alikamatwa na askari polisi waliokuwa eneo hilo na ndipo vurugu zikaanza na askari hao wanasemekana kuwasaidia POLISI WENZAO wakaanza kurusha mabomu katika eneo la jukwaa kuu ambako alikuwepo pia mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Stephen Masele ambaye pia ni naibu waziri wa madini hapa nchini.
Kufuatia
vurugu hizo baadhi ya watu waliokuwa eneo la jukwaa kuu akiwemo mbunge wa jimbo
la Shinyanga mjini Stephen Masele ambaye pia ni naibu waziri wa madini
wamejeruhiwa katika sehemu mbalimbali za miili yao.
Akizungumza
mara baada ya vurugu hizo naibu waziri wa madini Stephen Masele amesema vurugu
hizo zimetokana na askari polisi waliokuwa wanawasaidia polisi wenzao yaani
timu ya Polisi,walioshindwa kumdhibiti kijana aliyekuwa anakwenda kumsaidia refa.
Masele
amesema ni vyema TFF ikaaangalia namna ya kupunguza timu za polisi kwani ziko
nyingi sana na wanalindana matokeo yake kusababisha vurugu leo mjini Shinyanga
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ VURUGU ZATOKEA SHINYANGA,NAIBU WAZIRI WA MADINI STEPHEN MASELE APIGWA MABOMU WAKATI WA MCHEZO KATI YA STAND UNITED NA POLISI MARA.”
Post a Comment