Wednesday, May 21, 2014
BAADA YA KIKOMBE CHA BABU SASA NI DHAHABU SAMUNGE.
Do you like this story?
Maelfu ya watu wamemiminika tena katika eneo la
samunge wilaya ya ngorongoro mkoa wa aursha safari hii siyo kunywa kikoche cha
babu mchungaji ambilikile mwasapile bali
kupata dhahabu inayodaiwa kugundulika
katika eneo hilo.
Habari kutoka katika eneo hilo zinasema kuwa watu
wanazidi kumiminika katika kujipatia
madini hatyo yaliyobainika katika mashamba ya watu na maeneo ya kingo za mto
katika kijijji cha mgongo kilichopo jirani na kwa babu.
Diwani wa samunge Jackson sandea alisema maelfu ya watu kutoka maeneo
mbalimbali nchini wamefurika katika
kijiji ambacho kuna mto na madini ya dhahabu
yanapatikana hapo.
Hadi sasa kuna watu zaidi ya 4,000 na bado
wanaongezeka hii inaweza kuwa nai zaidi ya kipindi kile cha babu wa kikombe.
Dhahabu hii inapatikana mtoni tu watu
wanakusanya michanga na kupata dhahabu
hakuna mtu ambaye anachimba alisema sandea. Alisema tofauti na maeneo
mengine dhahabu ya samunge ina onekana ni ya watanzania wote kwani ipo eneo la
mto ambao unamilikiwa na serikali na ndiyo sababu wanaingia kwa wingi. Kuna
wenginawanapta hata mashambani lakini
mtoni ndipo inapoptikana kwa wingi zaidi alisema.
Ulinzi waimarishwa
Diwani huyo alisema ulinzi umeanz a kuimarishwa katika
eneo hilo akisema hali ikiachwa kama ilivyo kunaweza kutoke vurugu kubwa na
hata mauaji.
Sisi kama viongozi tumeweka utaratibu mzuri wa
kuchumba madini kiusalama na hata wale
ambao wameanza kuuza mashamba yao tunawawekea
utaratibu mzuri alisema.
Maofisa madini kutua samunge
Kamishna wa madini kamanda wa kaskazini alex magayane
alisema jana kwamba baada ya kupokea taarifa za kugundulika kwa dhahabu katika
eeno la samung maofis wake wanajidandaa kwenda kijijini hapo.
Alisema taarifa za kitaalamu kuhusu akiba ya madini
hayo iliyopo samunge itatolewa baada ya maofis hao kufika katika eneo hilo na
kufanya utafiti.
Ahadi ya babu
Kugundulika dhahabu katika eneo hilo kunahusishwa na
ahadi ya mchungaji msapila kuwa
mamilioni yawatu watafika tena samung e
bada ya kupungua ikilinganishwa na miezi ya mwanzao baada ya kuanza kutoa tiba
ya kikoche cha dawa iliyodaiwa kutibu mgonjwa sugu.
Licha ya wengi kuitilia shaka kauli yake hiyo
aliendelea kusisistiza na akakta miti na kujenga kituo kikubwa cha kutolea
huduma ya kikombe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BAADA YA KIKOMBE CHA BABU SASA NI DHAHABU SAMUNGE.”
Post a Comment