Friday, May 16, 2014
BARCELONA HAWATASHEREHEKEA UBINGWA WA LA LIGA.....NAO ATLETICO WATASHANGILIWA NA MASHABIKI 447 TU, MOTO UTAWASHWA KESHO YAKE.
Do you like this story?
Wanaume wa kazi kesho wanavaana na Barcelona |
Mashabiki wa Atletico Madrid watashangilia ubingwa wa La liga kwa saa 48 kama watatwaa kwa mara ya kwanza baada ya miaka 18 |
KAMA
Barcelona watashinda kesho dhidi ya Atletico Madrid na kutwaa taji la La Liga,
siku inayofuata hawatakuwa na sherehe ya kushangilia ubingwa ndani ya basi lao
la wazi na kupita mitaa ya Barcelona.
Hii
inatokana na kushindwa kuonesha makali msimu huu, hivyo wanaona hakuna haja ya
kufurahia mafanikio kiduchu namna hiyo.
Wachezaji,
makocha, wakurugenzi na mashabiki wa Barca walishakata tamaa ya kutwaa ubingwa
siku nyingi, kwahiyo kama watashinda kesho na kutwaa ubingwa wataondoka
uwanjani ndani ya muda mfupi.
Wachezaji
wa klabu hiyo wataondoka siku ya kesho yake na kwenda kujiunga na timu zao za
taifa kujiwinda na michuano ya kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
LA LIGA: PAZIA KUFUNGWA KESHO
Siku ya
mwisho kesho wapenzi wa soka watashuhudia Barcelona na Atletico wakichuana kwa
mara ya tatu katika historia yao.
Barcelona wataweza kushinda taji kutokana na rekodi nzuri ya `head-to-head` kama watawafunga Atletico Madrid.
Sare itatoshwa kuwapa Atletico ubingwa kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 18.
HEAD-TO-HEAD
21 August: Atletico 1-1 Barcelona
(Spanish Super Cup)
28 August: Barcelona 0-0 Atletico
(Spanish Super Cup)
11 January: Atletico 0-0 Barcelona
(La Liga)
1 April: Barcelona 1-1 Atletico
(Champions League)
9 April: Atletico 1-0 Barcelona
(Champions League)
Barcelona wataweza kushinda taji kutokana na rekodi nzuri ya `head-to-head` kama watawafunga Atletico Madrid.
Sare itatoshwa kuwapa Atletico ubingwa kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 18.
HEAD-TO-HEAD
21 August: Atletico 1-1 Barcelona
(Spanish Super Cup)
28 August: Barcelona 0-0 Atletico
(Spanish Super Cup)
11 January: Atletico 0-0 Barcelona
(La Liga)
1 April: Barcelona 1-1 Atletico
(Champions League)
9 April: Atletico 1-0 Barcelona
(Champions League)
Kama
Atletico Madrid watashinda taji kesho hakuna atakayelala ndani ya saa 48 ndani
ya mji mkuu wa Hispania.
Mshabiki
447 ndio waliopata tiketi za kushabikia timu ya Atletico hapo kesho, lakini
kama watashinda, moto utawashwa tena mapema jumapili nyumbani kwao Madrid.
Timu hizi
mbili zitashangilia ubingwa kwa staili tofauti kabisa. Wakatalunya watamfuta
kazi Kocha mkuu, Tata Maryino bila kujali kitakachotokea kesho jumamosi.
Mlinda
mlango Victor Valdes atajiunga na Monaco. Dani Alves atamfuata nchini
Ufaransa kwa kujiunga na PSG. Beki Carles Puyol atajiunga na kocha mpya
anayekuja, Luis Enrique kwenye benchi la ufundi.
Alex Song,
Javier Mascherano, Pedro na Alexis Sanchez wote wanauzwa na wanaweza kuondoka
kama ofa nzuri zitapatikana, huku Barcelona wakijiandaa kumsajili beki wa
Chelsea, David Luiz.
Barca
wanaweza kuwashawishi Chelsea kwa kuwapatia Alex Song na Alexis ili kuinasa
saini ya Luiz.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BARCELONA HAWATASHEREHEKEA UBINGWA WA LA LIGA.....NAO ATLETICO WATASHANGILIWA NA MASHABIKI 447 TU, MOTO UTAWASHWA KESHO YAKE.”
Post a Comment