Friday, May 30, 2014
SUALA LA WATENDAJI WA VIJIJI KUSOMA MAPATO NA MATUMIZI NI LA LAZIMA
Do you like this story?
Serikali imesema suala la watendaji
kusoma mapato na matumizi ya vijiji ama kata ni la lazima wala si hiyari yao
Kauli hiyo imetolewa bungeni Dodoma na
Naibu waziri Tamisemi Mh Agrey Mwanri katika kipindi cha maswali na majibu na
kuongeza kuwa kumekuwa na mtindo wa baadhi ya watendaji wa vijiji kukataa
kuwasomea wananchi mapato na matumizi wakidhani kuwa ndiyo utaratibu
Mh. Mwanri amesema ni lazima kila
mtendaji wa kijiji kuwasomea wananchi wake mapato na matumizi na taarifa hiyo
pia inatakiwa kubandikwa kwenye mbao za matangazo ili kila mwananchi aione kwa
wakati wake
Amesema kutosoma mapato na matumizi sio
tu kwamba ni kosa kisheria lakini pia linawakatisha tamaa wananchi kwa kuwa wao
ndio wanachanga fedha zao na wakiona hawasomewi mapato na matumizi wanadhani
kuwa fedha zao zimeliwa na wanakata tamaa ya kuchangia miradi ya maendeleo
Mh. Mwanri amesema hatua zitachukuliwa
kwa watendaji wa aina hiyo ambao hawasomi mapato na matumizi kwa wananchi hao
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SUALA LA WATENDAJI WA VIJIJI KUSOMA MAPATO NA MATUMIZI NI LA LAZIMA ”
Post a Comment