Friday, May 16, 2014
WANANCHI MBEYA WAONDOLEWA HOFU UGONJWA WA HOMA YA DENGUE.
Do you like this story?
Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Ndugu
Mariamu Mtunguja akitoa taarifa ya ugonjwa wa Dengue kwa waandishi wa habari
|
SERIKALI Mkoani
Mbeya, imewataka wakazi wa Mkoa wa Mbeya kuondoa hofu juu ya
ugonjwa ulioibuka nchini wa Dengue kwa kuwa mpaka sasa idara
ya afya haijapokea kesi ya mtu aliyepatwa na ugonjwa huo.
Akizungumzia
hilo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja, alisema hadi sasa hakuna
mtu au mgonjwa aliyeripotiwa kuwa na dalili za ugonjwa huo.
Mtunguja,
alilazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya kuzagaa kwa uvumi kutoka kwa baadhi ya
wananchi ya kwamba ugonjwa huo tayari umebisha hodi Mbeya na tayari kunamgonjwa
amelazwa.
Amesema taarifa
zilizoenea mtaani zinajengwa na hofu tu na kwamba timu ya wataalamu wa afya
imeendelea kufanya kazi muda wote ili kuona kama kuna taarifa za kuwepo au
kutokea kwa mtu yeyote mwenye dalili au ugonjwa huo.
Amesema tayari
madaktari wa wilaya zote mkoani hapa wamepewa waraka unaotoa muongozo wa
namna wa kushughulikia kwa haraka taarifa zote zinazotolewa na wananchi juu ya
mtu yeyote anayeonesha dalili za kuwa na ugonjwa wa Dengue.
Mbali na
madaktari, lakini pia ofisi hiyo ya Mkuu wa mkoa imetoa agizo kwa wakurugenzi
wa halmashauri zote kuhakikisha wanasimamia kwa nguvu zote suala la usafi.
Kwa upande
wake, Mganga Mfawidhi kutoka hospitali ya mkoa wa Mbeya, Dk. Grolia Mbwile,
alisema licha Tanzania kukumbwa na ugonjwa huo ambao hata hivyo hauna tiba wa
kinga, lakini pia umewahi kuibuka katika nchi ya Misri barani Afrika , pamoja
na nchi kadhaa katika bara la Asia.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa hivi karibuni na mtafiti wa tabia za mbu kutoka Taasisi ya
Afya ya Ifakara (IHI), Dk . Nicholaus Govela alisema ugonjwa wa Dengue
unaambukizwa na mbu aitwae Aedes Egypti.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANANCHI MBEYA WAONDOLEWA HOFU UGONJWA WA HOMA YA DENGUE.”
Post a Comment