Tuesday, June 3, 2014
MWIGULU KUPINGA BUNGE.
Do you like this story?
Mjadala wa bunge maalumu la katiba umeanza kuibuka upya wakati bunge la bajeti likienda ukingoni
ambapo naibu katibu mkuu wa CCM Tanzania bara mwigulu nchemba ameibuka na hoja
ya kupinga nyongeza ya siku 60 za bunge
hilo.
Akihutubia wakazi wa manispaa ya iringa na vitongoji
vyake katika mkutano uliopewa jina la
ondoa msigwa iringa mjini mwiguli amesema atapinga kwa nguvu zake zote bunge hili kukutana kwa
siku nyingine 60 wakati mwigulu akipinga kuendelea kwa bunge hilo mjumbe wa bunge hilo na mbunge kigoma kaskazini kabwe zitto ametuma ujumbe
kwa wajumbe wenzake walioujiundia kundi
la umoja wa katiba ya wananchi ukawa
kuwa ili kumuenzi mama yake mzazi shida
salum aliyefariki dunia juzi na kuzikwa
jana wawaletee watanzania katiba mpya.
Mwigulu ambaye pia ni naibu waziri wa fedha alisema
sababu ya hatua hiyo ni mtazamo wake
kuwa bunge hilo likiendelea kama
ilivyofanyika katika awamu ya kwanza
itakuwa sawa na kutumia vibaya fedha za
walipa kodi.
Akizungumzia muonekano wa bunge hilo uliofikia hatua
za baadhi ya wajumbe kuwakashifu waasisi
wa taifa mwigulu amesema natamani
siku moja niongoze taifa hili ili
niwafundishe watu kuwa na adabu.
Alisema katika mazingira ya kawaida inawezekana watoto wakatukanana lakini litakuwa jambo la ukosefu wa adabu kama
mtoto atamtukana baba yake.
Hawa watu wanaojiita ukawa hawna adabu wanapasea
kufundishwa adabu ni jambo la kushangaa
wnapoachwa tu wawatukane waaasisi wa
taifa hili alisema
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MWIGULU KUPINGA BUNGE.”
Post a Comment