Tuesday, June 3, 2014
WABUNGE WAMPOZA VICKY KAMATA.
Do you like this story?
WABUNGE wanawake wa bunge la muungano wamefanya hafla maalumu ya kumfariji mbunge mwenzao Vicky kamata aliyeugua ghafla
baada ya harusi yake kukwama kufungwa.
Vicky jana kwa mara ya kwanza tangu apate tatizo hili alionekana akishiriki vikao vya bunge huku akionekana mwenye afya
na mchangamfu kama kawaida yake .
Habari zinasema kuwa wabunge hao walitumia muda huo kumfariji lakini pia kumpongeza kwa
kushindwa kufunga ndoa hiyo kwa madai
kuwa hakuwa mume sahihi kwake.
Habari zaidi zinasema kuwa baadhi ya wabunge wanawake walizuiwa kushiriki hafla hiyo kwa madai
kuwa wamechangia kuvunjika kwa ndoa hiyo na kwamba walikuwa wakishangilia kukwama kwake
kwa sababu wanazozijua.
Wiki moja iliyopita mbunge huyo maarufu alitarajiwa kufnga ndoa na mchumba wake
Charles gardner lakini ilikwama kwa
madai ya kuwapo kwa kasoro za kisheria za kanisa katoliki.
Kukwama kufanyika kwa ndoa hiyo ilitarajiwa kutumia zaidi y ash milioni 96 kulisababisha
mbunge huyo kuugua ghafla na kulazwa katika hospitali ya general iliyopo tabata jijini dare s
salaam.
Ni matukio nadra kutokea katika maisha lakini haya ndiyo yaliyomkuta mbunge huyo
wa viti maalumu kupitia CCM baada
ya kuugua ghafla saa 36 kabla ya
harusi yake.
Vicky ilikuwa afunge ndoa jumamosi iliyopita katika
kanisa katoliki la parokia ya bikira maria mama wa mkombozi sinza dar es salaam
na tayari kadi za mailiko zilishasambazwa
kwa watu mablimbali wakiwamo wabunge.
Padre wa kanisa
katoliki parokia ya bikira maria mama wa mkombozi sinza Cuthbert maganga alipohojiwa kuhusu taaifa za kufunga kwa ndoa hiyo alikiri kwamba iliandikishwa
ili ifungwe kanisani hapo.
Hata hivyo akasema ilishindikana baada ya wahusika kukwama
kuwasilisha baadhi ya nyaraka muhimu zilizohitajika ili kukamilisha
sakramenti hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WABUNGE WAMPOZA VICKY KAMATA.”
Post a Comment