Tuesday, June 3, 2014
POLISI WANOLEWA UCHAGUZI MKUU WA 2015
Do you like this story?
. Harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015 zimeanza.
Polisi wameanza mafunzo yatakayowaongezea uwezo wa kusimamia uchaguzi huo.
Mafunzo
hayo yanafadhiliwa na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa
(UNDP), kupitia mradi wake wa Uwezeshaji wa Demokrasia (DEP).
Wakufunzi
wanane kutoka Chuo cha Polisi cha Uingereza wanaendesha mafunzo kwa maofisa 88
wa polisi wa ngazi za juu na kati.
Akizungumza
katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Naibu Kamishna wa Polisi, Simon Sirro amesema
yamekuja wakati mwafaka wakati jeshi hilo likijiandaa kwa shughuli hiyo muhimu
ya kitaifa.
Mafunzo
hayo yanayofanyika Dar es Salaam na Zanzibar yanalenga kuwajengea uwezo
makamanda wa polisi wa kupanga, kumudu na kuratibu kwa ufanisi hatua za
kipolisi za matukio yanayotishia utulivu wa amani katika jamii.
Amesema
katika kila kozi ambayo itaendeshwa kwa wiki mbili, itatoa mafunzo kwa maofisa
hao ya kuheshimu haki za binadamu, utawala wa sheria na namna ya kudhibiti
ghasia na baadaye kuwafundisha askari wote waliobaki. “Tunataka maofisa wetu
wawe na ujuzi wa kutosha kusimamia wakati wa vurugu ili uchaguzi ujao uwe wa
haki na amani. Wawe na uwezo mzuri wa kuwaelewesha wananchi juu ya kazi yao ili
kuendeleza imani juu ya polisi nyakati kama hizo. Pia yatatusaidia kutambua
namna gani tufanye kazi katika mazingira ya vurugu yenye watoto na wanawake.”
Alipoulizwa
juu ya matumizi ya nguvu nyingi kwa raia, Sirro alisema wasingependa polisi
kutumia nguvu hizo lakini mazingira husika hulazimisha hali hiyo kutokea.
Mtaalamu
wa masuala ya usimamizi wa uchaguzi wa UNDP nchini, William Hogan alisema
taasisi yake inathamini uchaguzi mkuu, pia namna polisi wanavyotumika katika
uchaguzi katika nchi za kidemokrasia. “Umakini wa polisi wakati wa usimamizi wa
uchaguzi hususan katika kuheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria ni moja
ya vitu muhimu ambavyo hupima iwapo uchaguzi husika ulikuwa wa haki na wazi
hivyo polisi wanahitajika kuongezewa uwezo,” amesema Hogan.
\
Amesema
mafunzo hayo ni mwendelezo tu wa mafunzo kwa polisi kwani yalishafanyika 2010
na yalikuwa na mafanikio.
Amesema
wanataka uchaguzi mkuu ujao uwe bora ulimwenguni kwa kuanzia na kuheshimu haki
za binadamu na utawala wa sheria.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “POLISI WANOLEWA UCHAGUZI MKUU WA 2015”
Post a Comment