Saturday, September 6, 2014
JESHI LA ZIMAMOTO LAKANUSHA KUWATIMUA ASKARI WANAFUNZI WENYE VIRUSI VYA UKIMWI.
Do you like this story?
WATU watano
wamehukumiwa kifungo cha miaka 37 jela na kuchapwa viboko 24 kila mmoja baada
ya kupatikana na hatia ya kuvamia na kupora fedha benki ya NMB tawi la Maswa
kwa kutumia silaha.
Hukumu hiyo ilitolewa
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Shinyanga na kusikilizwa na Hakimu
Mkazi wa Mahakama hiyo, Neema Gasabile ambapo alitoa hukumu hiyo.
Aliwahukumu kifungo
cha miaka 37 na viboko 24 kila mmoja viboko 12 wakati wa kuingia na 12 wakati
wa kutoka baada ya kuridhika na ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashitaka
kuwa kwa pamoja walitenda kosa hilo kinyume cha sheria.
Washitakiwa hao ni
Kapama Hamis Ramadhan (37), Mussa Athuman Buberwa (38), Amos Mathayo, Lucas
Vincent Mabela (40) na Zainabu Mchau (60) wote kwa pamoja walipatikana na hatia
ya makosa tisa ya jinai.
Mbele ya Hakimu mkazi
wa mahakama hiyo, Mwendesha Mashitaka Mwanasheria wa Serikali Edith Tuka
aliieleza mahakama hiyo kuwa washitakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa hilo
majira ya saa 6:00 mchana Julai 5, mwaka 2010 mjini Maswa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “JESHI LA ZIMAMOTO LAKANUSHA KUWATIMUA ASKARI WANAFUNZI WENYE VIRUSI VYA UKIMWI.”
Post a Comment