Tuesday, November 4, 2014

KOCHA MKUU WA TAIFA STARS NOOIJ KUTANGAZA KIKOSI KESHO




Na Boniface Wambura, Dar es salaam
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij kesho (Novemba 5 mwaka huu) atatangaza kikosi cha timu hiyo kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) itakayochezwa ugenini Novemba 16 mwaka huu.

Nooij atatangaza kikosi hicho mbele ya waandishi wa habari katika mkutano utakaofanyika saa 4.30 asubuhi kwenye ofisi za TFF zilizoko ghorofa ya tatu, Jengo la PPF Tower jijini Dar es Salaam.


Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Swaziland, mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Somhlolo jijini Mbabane.

0 Responses to “KOCHA MKUU WA TAIFA STARS NOOIJ KUTANGAZA KIKOSI KESHO”

Post a Comment

More to Read