Wednesday, December 16, 2015

MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO ATOA CHANGAMOTO KWA TCRA




NA SAMWEL NDONI, MBEYA
MKUU wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amelitaka baraza la ushauri la watumiaji wa huduma za mawasiliano Tanzania (TCRA-CCC), kubuni na kuweka mikakati mizuri itakayoboresha huduma za mawasiliano  ili kuendana na kasi ya ongezeka la watumiaji wa mawasiliano nchini.

Kandoro amesema kuwa kumekuwepo na ongezeko la watumiaji wa simu za kiganjani kutoka watu miliioni 28, mwaka jana hadi kufikia watu milioni 33 mwezi mwachi mwaka huu.

Akizungumza wakati akizindua semina ya siku moja ya kuelimisha watumiaji wa huduma za mawasiliano nchini iliyoandaliwa na TCRA-CCC, alisema kuwa baraza hilo lina wajibu wa kubuni njia na kuweka mikakati ili kutoa huduma kwa watumiaji wa mawasiliano  itakakayoendana na ukuaji wa sekta hiyo.

Hata hivyo aliwataka wanafunzi wa vyuo mbalimbali nchini kutumia teknolojia ya mawasiliano ya intaneti kwa kujiongezea uelewa ili kuendana na changamoto za dunia badala ya kutumia kupekua mitandao ya kijamii ambayo haina faida.

Amesema kuwa ikiwa wanafunzi watutumia vizuri mitandao kwa kujisomea itawajengea uwezo wa kuelewa mambo mbalimbali na  kinyume na hapo taifa litaendelea kuwa kizazi kisichokuwa na maadili kutokana na matumizi mabaya ya mtandao.

Mwenyekiti wa TCRA-CCC, Stanley Mwabulambo alisema semina hiyo imewashirikisha wadau mbalimbali wa mawasiliano wakiwemo wanafunzi wa vyuo TEKU, Tumaini, MUST, TIA Mzumbe, wawakilishi kutoka mamlaka ya udhibiti wa nchi kavu na majini Sumatra, jeshi la polisi, mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA, vikundi, asasi, taasisi na wadau wengine.

Amesema kuwa lengo la semina hiyo ni kuelimisha, kuhamasisha na kutambua changamoto za watumiaji wa mtandao sambamba na kuelimisha watumiaji hao juu ya matumizi sahihi ya mtandao.
MWISHO





.

























































































0 Responses to “MKUU WA MKOA WA MBEYA ABBAS KANDORO ATOA CHANGAMOTO KWA TCRA”

Post a Comment

More to Read