Thursday, December 24, 2015
POLISI WAAGIZWA KUWAKAMATA WAENDESHA PIKIPIKIWOTE WANAOKIUKA SHERIA
Do you like this story?
Jeshi
la Polisi limeagiza maaskari nchi nzima kufanya operesheni maalum ya kuwakamata
madereva bodaboda na abiria wanaukubali kupanda zaidi ya wawili-maarufu
mishikaki- na wanaopita katika ya magari na kuwasweka rumande kabla ya
kuwafungulia mashtaka ya kuvunja sheria ya usalama barabarani.
Akitoa agizo
mbele ya waandsihi wa habari, msemaji wa jeshi la Polisi makao makuu ya Polisi
SSP Advera Bulimba amesema opereshani hiyo itaenda sambamba na kuwakamata
madereva bodaboda wanaohatarisha maisha ya wananchi na vyombo vya usafiri
kwa kupita katikatio ya magari, pamoja na madereva walevi.
Kuhusu siku kuu
ya Maulid, X-mas na mwaka mpya, amesema jeshi la Polisi limewataka wananchi
kutoa taarifa mapema iwapo wanaona sura ya watu wasioeleweka katika maeneo yao,
pamoja na viashiria vingine vya uvunjifu wa amani ili ziweze kuchukuliwa hatua
za haraka ambapo amewataka wamiliki wa kumbi za starehe kutojaza watu kupita
kiasi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
.gif)


0 Responses to “POLISI WAAGIZWA KUWAKAMATA WAENDESHA PIKIPIKIWOTE WANAOKIUKA SHERIA”
Post a Comment