Monday, January 4, 2016

TFF KATIKA TUHUMA NYINGINE NZITO, ACHANA NA ILE YA KUKWEPA KODI




Kweli soka la bongo ni kizungumkuti, waamuzi wanaochezesha liki kuu ya Voidacom Tanzania bara wamefichua ‘jipu’ jingine ndani ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) safari hii siyo lile la kudaiwa kodi na TRA bali jipu hili ni la kudaiwa posho na baadahi ya waamuzi wa VPL.

Waamuzi waliochezesha mchezo kati ya Coastal Union dhidi ya Stand United uliochezwa December 26, 2015 hawajapewa posho zao hadi sasa huku waamuzi hao wakitakiwa kujigharamia usafiri, chakula pamoja na malazi.

Mtendaji mkuu wa bodi ya ligi Boniface Wambura kupitia gazeti moja la michezo alikanusha taarifa za bodi yake kudaiwa na waamuzi hao, akisema hakuna mwamuzi anayeidai bodi yake.

Mmoja wa waamuzi ambaye ni miongoni mwa waliochezesha mechi ya Coastal Union vs Stand United amezungumza na mtandao huu kwa sharti la kutoandikwa jina lake amemesema bado hawajalipwa pesa za mchezo huo uliochezwa tarehe 26. 12. 2015.

“Nimesoma gazeti la Champion, Wambura anasema hakuna referee anayedai lakini mpaka leo sisi hatujalipwa tumechezesha mchezo kati ya Coastal Union na Stand United tarehe 26. 12. 2015”, alisema mwamuzi huyo ambaye alitoa tahadhari ya kutoandikwa jina lake.

Kwa mwenendeno huu, je TFF inaweza kupambana na suala waamuzi kupokea rushwa na upangaji matokeo?

0 Responses to “TFF KATIKA TUHUMA NYINGINE NZITO, ACHANA NA ILE YA KUKWEPA KODI”

Post a Comment

More to Read