Tuesday, January 5, 2016
WAAFRIKA TUMEJALIWA SANA MIPANGO, HEBU CHEKI PLAN ZA CECAFA MWAKA 2016
Do you like this story?
![]() |
Shirikisho
la vyama vya soka vya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limetangaza programs
ambazo zitasaidia kukuza soka la nchi za ukanda huo.
Kikao
cha kwanza cha bodi tangu kufanyika kwa uchaguzi kilichoongozwa na rais wa
CECAFA Dr. Mutasim Gafaar kwenye mji wa Khartoum kimefikia maadhimio
kadhaa, kamati kuu imepitisha mikakati mipya ambayo imebeba mipango ya program
za maendeleo.
Michuano
miwili ya U-17 kwa wanaume na wanawake itafanyika mwaka 2016 kama inavyooneshwa
kwenye mipango mipya iliyopitishwa na shirikisho linalosimamia soka la Afrika.
Mikakati
mingine ya maendeleo ambayo utekelezaji wake utaanza mwaka 2016 ni mafunzo kwa
makocha, waamuzi, beach soccer (soka la mchangani) pamoja na mafunzo ya utawala
kwa ajili ya kujenga nguvu ya CECAFA.
CECAFA
ambayo ndiyo chama cha soka chenye michuano mikongwe Afrika kimedhamiria
kuongeza nguvu yake kwenye soka na kuwavutia wawekezaji kwa kuboresha
mashindano pamoja na mambo mengine ya kimaendeleo.
“Kamati
kuu inatambua uhitaji na umuhimu wa wadhamini na kwasababu hiyo, tumeamua
kutafuta wadhamini kwa ajili ya michuano yetu”, alisema makamu wa rais wa
CECAFA Abdiqani Said Arab baada ya kikao cha kamati kuu.
Alisema
pia, shirikisho hilo litaimarisha uhusiano na ushirikiano na vyama pamoja na
mashirikisho mengine ya soka ulimwenguni.
Kama
mipango na mikakati hiyo itafanikiwa kutekelezwa, huo utakuwa ni mwanzo wa
kutimia kwa ndoto za CECAFA za muda mrefu lakini pia utakuwa ni mwanzo mzuri
kwa uongozi uliochaguliwa chini ya Dr. Mutasim Gafaar wa Sudan.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
.gif)


0 Responses to “WAAFRIKA TUMEJALIWA SANA MIPANGO, HEBU CHEKI PLAN ZA CECAFA MWAKA 2016”
Post a Comment