Friday, August 12, 2016

KOCHA MKENYA ASHIKWA AKICHUKUA SAMPULI KWA NIABA YA MCHEZAJI





Kenya imeingia tena kwenye vichwa vya habari baada ya  Kocha wa timu ya riadha ya Kenya inayoshiriki michuano ya Olimpiki mjini Rio de Janeiro kurudishwa nyumbani kwa kosa la udanganyifu.

Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya kenya, Kip Keino amesema John Anzrah aliigiza kama miongoni wa wakimbiaji wa mita 800, na kutoa sampuli ya mkojo kwa niaba ya mkimbiaji Ferguson Rotich.

Udanganyifu huu uligundulika pale lilipofika swala la  picha za kitambulisho  ndipo walipogundua kuwa sura ya Bw Anzrah haeindani na mchezaji aliyefanya uchunguzi.

Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya Kenya, Kipchoge Keino amesema uongozi wa timu yake hautavumilia tabia hiyo ingawa mpaka sasa hakuna hatua yoyote iliyotolewa dhidi ya Rotich.

Anzrah ni afisa wa pili kutoka kenya kurejeshwa nyumbani, wa kwanza akirudishwa kwa kosa la kuomba rushwa ili kuweza kukwepa upimaji wa matumizi ya dawa za kusisimua misuli.

Kumekuwa na idadi kadhaa ya wanariadha wa Kenya ambao walishindwa kufuzu vipimo vya matumizi ya dawa za kuongeza nguvu huku ni wiki iliyopita tu shirika la kupambana na matumizi ya dawa hizo WADA likiiondoa Kenya kwenye nchi zilizoshindwa kutimiza masharti

Chanzo: BBC 

0 Responses to “KOCHA MKENYA ASHIKWA AKICHUKUA SAMPULI KWA NIABA YA MCHEZAJI”

Post a Comment

More to Read