Friday, August 12, 2016
KOCHA MKENYA ASHIKWA AKICHUKUA SAMPULI KWA NIABA YA MCHEZAJI
Do you like this story?
Kenya imeingia tena kwenye vichwa vya habari baada ya Kocha wa timu ya riadha ya Kenya
inayoshiriki michuano ya Olimpiki mjini Rio de Janeiro kurudishwa nyumbani kwa
kosa la udanganyifu.
Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya kenya,
Kip Keino amesema John Anzrah aliigiza kama miongoni wa wakimbiaji wa mita 800,
na kutoa sampuli ya mkojo kwa niaba ya mkimbiaji Ferguson Rotich.
Udanganyifu huu uligundulika pale lilipofika swala la picha za kitambulisho ndipo walipogundua kuwa sura ya Bw Anzrah haeindani na mchezaji aliyefanya
uchunguzi.
Mkuu wa Timu ya Olimpiki ya Kenya,
Kipchoge Keino amesema uongozi wa timu yake hautavumilia tabia hiyo ingawa
mpaka sasa hakuna hatua yoyote iliyotolewa dhidi ya Rotich.
Anzrah ni afisa wa pili kutoka kenya
kurejeshwa nyumbani, wa kwanza akirudishwa kwa kosa la kuomba rushwa ili kuweza
kukwepa upimaji wa matumizi ya dawa za kusisimua misuli.
Kumekuwa na idadi kadhaa ya
wanariadha wa Kenya ambao walishindwa kufuzu vipimo vya matumizi ya dawa za
kuongeza nguvu huku ni wiki iliyopita tu shirika la kupambana na matumizi ya
dawa hizo WADA likiiondoa Kenya kwenye nchi zilizoshindwa kutimiza masharti
Chanzo: BBC
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KOCHA MKENYA ASHIKWA AKICHUKUA SAMPULI KWA NIABA YA MCHEZAJI”
Post a Comment