Wednesday, November 2, 2016

SIMBA YAENDELEA KUONYESHA UBABE YAMNYUKA STAND KAMBARAGE




Simba SC imevunja rekodi ya Stand United ya kutofungwa kwenye uwanja wao wa nyumbani kwenye msimu huu, baada ya kuichapa kwa bao 1-0 kwenye uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Shiza Kichuya aliifungia alikwamisha bao pekee kwenye mchezo huo lililoipa Simba pointi tatu dhidi ya Stand United.
Awali Stand United walikuwa hawajapoteza mchezo kwenye uwanja wao wa nyumbani, walipoteza mchezo wao wa kwanza kwenye ligi msimu huu waliposafiri kuifuata Tanzania Prisons ambapo walifungwa bao 2-1 kwenye uiwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

0 Responses to “SIMBA YAENDELEA KUONYESHA UBABE YAMNYUKA STAND KAMBARAGE”

Post a Comment

More to Read