Wednesday, March 29, 2017

ATUPWA JELA MIAKA 5 KWA KUMFUNGA MBWA WAKE KAMBA MDOMONI


Mwanamume mmoja alietambulika kwa jina la William Dodson (43) raia wa Marekani ambaye alimfunga mbwa wake mdomoni kwa kamba, amehukumiwa kifungo cha miaka mitano jela.
Anasema alimfunga mbwa huyo mdomoni kwa sababu alibweka sana ndipo alipoamua kufunga mbwa huyo mpaka kumsababishia kupoteza sehemu ya ulimi wake. , jambo ambalo lilisababisha mbwa huyo kufanyiwa upasuaji mara kadha.
Kamba aliyotumia kumfunga mbwa hiyo ilizuia damu kufika hadi kwenye ulimi wake, na iliwachukua madaktari wa mifugo karibu saa 36 kuiondoa.
Mbwa huyo aliyejulikana kwa jina la Caitlyn, alifanikiwa kutoroka mwezi Mei mwaka 2015, na alikuwa mgonjwa sana wakati alipatikana akirandaranda barabarani
Caitlyn, alikuwa na umri wa miezi 15 wakati alipatikana na sasa amehitimu miaka mitano akiwa anaishi na familia tofauti.
Wakati huo chama cha wanyama cha Charleston, kibadilisha picha ya akaunti yake na kuweka picha ya mbwa hiyo, kama njia ya kuonyesha uzalendo.

0 Responses to “ATUPWA JELA MIAKA 5 KWA KUMFUNGA MBWA WAKE KAMBA MDOMONI”

Post a Comment

More to Read