Wednesday, March 29, 2017

WAKAZI WA NJOMBE WAHIMIZWA KUCHANGIA DAMU


Katibu Tawala wilaya ya Njombe, Joseph Chota amewahimiza wakazi wa mkoa wa Njombe kujitolea kuchangia damu salama ili kusaidia watu wenye mahitaji.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa katika maadhimisho ya wiki ya matendo ya huruma ya kanisa la Waadventista Wasabato mkoni Njombe, Chota amesema damu itakayochangwa pia itasaidia kukabiliana na tatizo la uhaba wa damu salama katika bohari za dawa hospitalini.

Waumini wa kanisa la Waadventista Wasabato Duniani kote huadhimisha siku ya matendo ya huruma kwa kuisaidia jamii kutatua changamoto mbalimbali ikiwa ni sehemu ya ibada na kumtukuza Mungu.

0 Responses to “WAKAZI WA NJOMBE WAHIMIZWA KUCHANGIA DAMU”

Post a Comment

More to Read