Wednesday, March 29, 2017

KAMATI TA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA IRINGA YAVAMIA BWAWA LA MTERA


Halmashauri ya wilaya ya Iringa kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo wamefanya msako wa kukamata nyavu aina ya Makokoro zinazotumika kuvua samaki wadogo wasioruhusiwa kuvuliwa katika bwawa la Mtera mkoani Iringa na kufanikiwa kukamata zana haramu za uvuvi 60 watuhumiwa 12 na kilo za samaki wadogo wakavu na wabichi 1227.

Msako huo ulioanza majira ya saa kumi alfajiri umewajumuisha jeshi la polisi wakiongozwa na mkuu wa polisi wilaya ya Iringa pamoja na ofisi ya mshauri wa mgambo wilaya umelenga kukamata samaki wadogo wanaovuliwa kinyume cha sheria katika bwawa hilo kama anavyofafanua kiongozi wa operesheni hiyo Joseph Chitinka ambaye ni mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Iringa.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya Iringa Bibi Lucy Nyalu anasema operesheni hii ni endelevu kwa lengo la kukomesha matumizi ya zana zisizostahili katika shughuli ya uvuvi katika eneo lake huku afisa uvuvi kata ya migori baraka uchimbira akiwataka wavuvi hao kukata leseni ili kufanya shughuli hiyo kihalali na kuepuka usumbufu.

0 Responses to “KAMATI TA ULINZI NA USALAMA YA WILAYA IRINGA YAVAMIA BWAWA LA MTERA”

Post a Comment

More to Read