Friday, March 31, 2017

SIKILIZA SAUTI:WAZIRI MKUU ATEMA CHECHE KATIKA JIMBO LA RIDHIWANI




 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametembelea Wami katika Jimbo la Chalinze kufuatilia na kukagua maendeleo ya mradi wa maji wa Jimbo hilo ambapo Mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete amekuwa akiulalamikia kwa muda mrefu kwa niaba ya wakazi wa Chalinze.
Katika ziara hiyo Waziri Mkuu ambaye alitembelea Wami, Miono na Saadan alitoa siku 100 kwa Mkandarasi wa mradi wa usambazaji wa maji Chalinze kuukamilisha mradi huo angalau kwa asilimia 80 ikiwemo ujenzi wa matanki 17 ya kuhifadhi maji kabla ya May 31 mwaka huu baada ya mradi huo kusuasua.

0 Responses to “SIKILIZA SAUTI:WAZIRI MKUU ATEMA CHECHE KATIKA JIMBO LA RIDHIWANI ”

Post a Comment

More to Read