Wednesday, June 11, 2014
SHILINGI 11 BILLIONI ZA SAFARI ZA JK ZAFYEKWA.
Do you like this story?
Bajeti y ash 50 billioni
zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya safari ya rais jakaya kikwete
katika mwaka ujao wa fedha ni
miongoni mwa mafungu ya fedha yaliyopigwa panga ili kuwezesha kupatikana kwa fedha
za kugharamia miradi ya maendeleo.
Habari kutoka ndani ya kikao
cha majadiliano baina ya serikali na kamati ya bunge ya bajeti zinasema sh 11 bilioni zimepunguzwa katika fungu hilo
na kubakiza sh 39 bilioni.
Hata hivyo kiasi
kilichobakishwa ni ongezeko la asilimia j260
la sh 15 bilioni zilizopitishwa na bunge mwaka jana kwa ajili ya safari
za rais katika mwaka wa fedha unaomalizika june 30 mwaka huu.
Kwa hiyomwaka 2014/15
serikali ilimtengea rais sh 50 billioni za safri ila tumekata sh bilioni
11 ili kupeleka katika shughuli zingine
za maendeleo kwa hiyo kwa mwka ujao wa
fedha safari za rais zitatengwa sh 39 bilioni.
Awali ilielezwa kuwapo kwa
mvutano mkali baina ya serikali
na kamati ya bunge la bajeti lakini jana mchan apande hizo zilikubaliana
kukata asilimia 7.5 ya fedha katika baadhi ya mafungu ya matumizi mengineyo
(oc) kutoka katika wizara zote ili
kuwezesha kupatikana kwa sh 230 bilioni
ambazo zinahitajika kwa ajili ya
maendeleo hata katika sekta tatu afya, miundombinu, na kilimo.
Bado kikao kinaendelea na
tangu asubuhi tumekata fedha katika fungu la matumizi mengineyo mfano chai katika
ofisi zawizara
pamoja na ununizi wa magazeti ununuzi wa magari ya kifahari mafuta viburudisho semina na makongamano pamoja na sagari za ndani kilieleza chanzo
chetu.
Juzi naibu waziri wa fedha
mwigulu nchemba alisema wizara yake inakusudia
kupitia bajeti za wizara zote ili
kuhamisha yasiyo ya lazima ili
zielezwe katika mahitaji muhimu.
Kwa wananchi wanakula mlo
mmoja kwa siku waliopo wizarani
hawawezi kufa kwa kukosa chai
hasubuhi tutafanya hivyo ili fedha hizo
zipelekwe katika shughuli za maendeleo.
Kesho(jana) katika kikao cha
mashauriano tutakwenda kuweka msimamo wa pamoja katika jambo hilo wizzara
zisielekeze macho wizara ya fedha pekee
nazo zinatakiwa kuwa na miakakti ya kubana matumizi yake.
Mwenyekiti wa kamti ya bunge
la bajeti Andrew change alipoulizwa kuhusu hatua iliyofikiwa katika majadiliano alisema siburini itakaposomwa bajeti mtajua
kilichoamuliwa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SHILINGI 11 BILLIONI ZA SAFARI ZA JK ZAFYEKWA.”
Post a Comment