Monday, December 22, 2014
TWIGA CEMENT YAZINDUA CHAMA CHA MAKIPA TANZANIA. TASWA FC WAFUNGUA NJIA.
Do you like this story?
Kampuni ya
Twiga Cement ya jijini Dar es Salaam, jana imefanikiwa kuzindua rasmi Chama cha
Wachezaji wa Nafasi ya Golikipa wanaoshiriki ligi kuu ya Vodacom Tanzania,
ambapo katika uzinduzi huo timu hiyo ya Makipa ilicheza mchezo wa Kirafiki
dhidi ya Timu ya Kombaini ya Waandishi wa Habari TASWA F.C.uliofanyika kwenye
Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar es Salaam jana.
Katika mchezo
huo ambao ulikuwa na Ushindani wa Kipekee kutokana na Timu zote kuwa na
Wachezaji Nyota na Tegemeo katika Vipaji vyao, Mashabiki waliofika kushuhudia
mchezo huo walifurahishwa na jinsi kila mchezaji alivyoonyesha Ujuzi binafsi na
kiwango cha hali ya juu. Timu ya makipa ndiyo iliyokuwa ya kwanza kufanya shambulizi kwenye lango
la timu ya TASWA ambapo dakika ya 26 mchezaji Shaaban Kado alikosa Penalt
kutokana na beki wa Taswa Martin Peter kunawa akiwa eneo la kumi na nane na
penalt hiyo ilidakwa na kipa nyota wa TASWA Ahmed Famau.
Hadi kipindi
cha kwanza kinamalizika kikosi cha timu ya Makipa kilikuwa mbele kwa bao
1-0,lililofungwa na Juma Kaseja baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa
TASWA, ambapo kipindi cha pili kila timu ilifanya mabadiliko ambapo Taswa
iliwatoa, Majuto Omary, Ibrahim Masoud, Ally Mkongwe, Zahoro Mlanzi, Shafii
Dauda, na nafasi zao kuchukuliwa na Salum Jaba, Juma Ramadhani, Hatibu
Naheka,na Paul Limoy,mabadiliko ambayo hata hivyo yalishindwa kupunguza kasi ya
wachezaji hao Makipa wa Ligi kuu waliokuwa muda wote wakilisakama lango la
TASWA FC.
Pamoja na
kuwa na wachezaji wa akiba timu ya Makipa lakini walishindwa kufanya
mabadiliko, kutokana na wachezaji wengi kuwa na pumzi ya kuwamudu TASWA ambapo
Makipa hao walisaidiwa na mlinda mlango kutoka timu ya Taifa ya Wanawake Twiga
Stars, Fatuma Omary ambaye hata hivyo alionyesha kiwango kikubwa baada ya
kudaka michomo ya wazi kutoka kwa washambuliaji wa Taswa,Ibrahim Masoud, Shafii
Dauda,Majuto Omary pamoja na Ally Mkongwe waliokuwa wakilisakama Lango la timu
ya makipa kila wakati.
goli la pili
lilipatikana kunako dakika ya 67 kupitia kwa Ivo Mapunda aliyefunga kwa shuti
kali lililomshinda mlinda wa TASWA Ahmed Famau,kabla ya shaaban Kado
kuhitimisha Kapu la Magoli kwa timu hiyo ya Makipa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “TWIGA CEMENT YAZINDUA CHAMA CHA MAKIPA TANZANIA. TASWA FC WAFUNGUA NJIA. ”
Post a Comment