Saturday, January 3, 2015
DAVID MWAMWAJA AITAMANI NDANDA FC
Do you like this story?
Kocha mkuu wa
Tanzania Prisons David Mwamwaja amesema ana kiu ya kuchukuwa pointi
tatu katika uwanja wake wa nyumbani kesho.
Akizungumza
mara baada ya mazoezi katika uwanja wao wa magereza ,Mwamwaja alisema
kuwa baada ya kutoka suluhu na wagosi wa kaya Coastal Union mechi
iliyopita,sasa wamejipanga kufunguka katika mechi ya Ndanda jumapili katika
uwanja wa Sokoine jijini hapa.
“Tumefanyia
kazi makosa yaliyojitokeza tulipo cheza na Coastal hasa katika safu ya
umaliziaji tatizo ambalo limekuwa likiisumbua timu yangu lakini kwasasa
limeisha”alisema Mwamwaja.
Timu hiyo
ambayo kwasasa imeongeza mda wa mazoezi kutoka dakika 120 hadi dakika 240 ili
kuendelea kujiimarisha zaidi.
Tanzania
Prisons kwasasa ipo katika nafasi ya 13 kati ya timu 14 zinazo shiriki ligi kuu
Tanzania Bara ambapo jumapili hii itashuka dimbani na timu ya Ndanda Fc
ya Mtwara.
Mwisho
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “DAVID MWAMWAJA AITAMANI NDANDA FC”
Post a Comment