Thursday, March 13, 2014

BREAKING NEWS: SAMIA SULUHU HASSAN ACHAGULIWA RASMI KUWA MAKAMU MWENYEKITI WA BUNGE LA KATIBA.




Hatimaye bunge maalum la katiba limemchagua Mh. Samia Suluhu Hassan kuwa makamu mwenyekiti wa bunge hilo, katika uchaguzi huo uliofanyika muda huu bungeni Dodoma

Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi huo amesema Mh. Samia amepata kura 390 sawa na asilimia 74.6 huku mgombea mwenzake Mh. Amina Abdalah Amour akipata kura 126, ambapo kura 7 zimeharibika

Kwa matokeo hayo Mh Samia amekuwa makamu mwenyekiti mteule wa bunge maalum la katiba

Akizungumza mara baada ya kutangazwa, Mh. Samia amesema anamshukuru mpinzani wake kwa kumpa wakati mgumu ikiwemo kigezo cha kukubalika ndani ya bunge, pamoja na wanawake wote waliopo ndani ya bunge hilo kwa kumpa ushindi huo

Awali Mh. Amina yeye amekubaliana na matokeo hayo, na kuongeza kuwa kwa kuwa aliyeshinda ni mwanamke, basi ushindi huo ni wa wanawake wote

0 Responses to “BREAKING NEWS: SAMIA SULUHU HASSAN ACHAGULIWA RASMI KUWA MAKAMU MWENYEKITI WA BUNGE LA KATIBA.”

Post a Comment

More to Read