Monday, March 31, 2014
JELA MIEZI SITA KWA WIZI WA JENEZA.
Do you like this story?
Mahakama ya Wilaya ya Bariadi, mkoani
Simiyu imemhukumu Bahati Lukas (25) kifungo cha nje miezi sita baada ya
kupatikana na hatia ya wizi wa jeneza.
Mwanamke huyo mkazi wa kijiji cha Nyaumata,
Kata ya Somanda mjini Bariadi alihukumiwa kifungo hicho baada ya kukiri.
Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Inspekta Samwel
Kilabuka alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo Machi 19 mwaka huu eneo la
Somanda.
Alidai mshtakiwa alifika maeneo yanapochongwa
na kuuzwa majeneza hayo na aliulizia bei ya jeneza ili auziwe.
Kilabuka alidai mshtakiwa baada ya kuambiwa
bei ya jeneza alisimama, huku muuzaji akiendelea na shughuli nyingine. Inadaiwa
hatua hiyo ilitoa nafasi kwa mshtakiwa kubeba jeneza hilo kichwani na kutoweka
nalo.
Baada ya kusomewa shtaka hilo, mshtakiwa
alikiri kutenda kosa, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya, Robart Oguda
alimhukumu kifungo cha nje miezi sita.
Hakimu Oguda alisema mahakama ilibaini
mshtakiwa alikuwa na matatizo ya akili, ikiwamo pia ugumu wa hali ya maisha
yake
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “JELA MIEZI SITA KWA WIZI WA JENEZA.”
Post a Comment