Monday, March 31, 2014
RAZA: TUACHE UTOTO TUJADILI KATIBA.
Do you like this story?
Mjumbe wa Bunge la Katiba, Mohamed Raza
ametaka wajumbe wenzake kuheshimiana bila kujali wingi au uchache wa wajumbe
kwenye makundi yao, kama kweli wana dhamira ya dhati ya kutunga Katiba.
Akizungumza na gazeti hili, Raza alisema
mwenendo wa Bunge siyo mzuri na hauleti picha nzuri kwa mamia ya wananchi ambao
wanategemea wapatiwe Katiba bora itakayoondoa tatizo yao.
“Tupo hapa tunalipwa kwa siku Sh.300,000 na
tunajua huku nyuma kuna maelfu ya wananchi wetu hawana hata Sh.1000 ya chakula,
halafu tunakaa hapa tunafanya vurugu na kuacha kusikilizana hata katika hoja za
msingi? Nadhani hatuwatendei haki wananchi,” alisema Raza.
Amesema hakuna asiyejua matatizo ya wananchi.
Kinachotakiwa sasa ni kukaa na kuanza kupitia Rasimu ya Katiba, hasa baada ya
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba kuiwasilisha
bungeni.
“Hakuna ambaye alizaliwa na mama yake na
kuelezwa ipo siku atashiriki kuandika Katiba ya mamilioni ya wananchi wa
Tanzania. Sasa hii ni fursa nzuri kwetu sote kukaa na kutafakari matatizo yetu
na kuyapatia ufumbuzi katika katiba hii mpya,” alisema Raza.
Aidha amesema ni muhimu kujadili Rasimu ya
Katiba katika muktadha wa kiuchumi ili kuhakikisha inakwenda kwa wananchi na
kukubalika na siyo kutanguliza masilahi ya kisiasa au makundi wanayotoka
wajumbe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RAZA: TUACHE UTOTO TUJADILI KATIBA.”
Post a Comment