Monday, March 31, 2014
KIBADENI AJIGAMBA, ASEMA KUSHUKA NO.
Do you like this story?
Kocha wa Ashanti United, Abdallah Kibadeni amesema atahakikisha timu
yake inashinda mechi zake zilizobakia za Ligi Kuu ili wasishuke.
Kibadeni
alisema hayo baada ya kuiongoza Ashanti kuichapa JKT Oljoro kwa mabao 2-0 juzi
kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Matokeo
hayo yaliiwezesha Ashanti kufikisha pointi 21 na kukamata nafasi ya 11, huku
wakiishusha Mgambo Shooting yenye pointi 19 mpaka katika nafasi ya 12.
Ashanti
sasa ina mechi tatu mkononi dhidi ya Mbeya City itakayopigwa Jumamosi hii
kwenye Uwanja wa Azam Complex, Simba itakayoumana nayo Aprili 13 na Tanzania
Prisons itakayopigwa Aprili 19 kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Kibadeni
alisema ushindi alioupata dhidi ya JKT Oljoro umeongezea morali kwa kikosi
chake kutaka kufanya vizuri zaidi ili kucheza Ligi Kuu msimu ujao.
“Hivi
sasa hatuna muda wa kupoteza zaidi ya kuhakikisha tunashinda mechi mechi zote
zilizobaki ili tucheze Ligi Kuu msimu ujao.
“Ni
kazi ngumu kwa sababu mechi zote zilizobaki ni ngumu, lakini naamini kwa morali
waliyonayo wachezaji wangu tutashinda,” alisema Kibadeni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KIBADENI AJIGAMBA, ASEMA KUSHUKA NO.”
Post a Comment