Monday, March 31, 2014
JUMLA YA SHILINGI MILION 37,410,000 ZIMEPATIKANA KATIKA MECHI YA MBEYA CITY &TANZANIA PRISONS.
Do you like this story?
![]() |
Kikosi cha Timu ya Mbeya City kikiwa katika mazoezi kabla ya Mechi na Tanzania Prisons |
![]() |
Timu ya Tanzania Prisons ikiwa katika Mazoezi kabla ya Mechi. |
JUMLA ya shilingi
milioni 37,410,000 zimepatikana katika mechi ya Mbeya City na Tanzania
Prisons iliyochezwa juzi katika uwanja wa kumbukumbu wa Sokoine huku timu
ya Mbeya City ikiondoka na ushindi wa goli 1-0.
Akisoma mapato hayo Katibu wa
chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA) Selemani Harubu , alisema kati
mapato hayo shilingi milioni 8,467,499 zimeenda kwa kila timu.
Alisema, gharama ya Vat ni shilingi
milioni 5,705610 tiketi shilingi 3,00,000 gharama ya mchezo
2,583,305huku kamati ya ligi ikiondoka na shilingi 2,883,305.
Alisema, TFF imepata
shilingi 1,291652 na MREFA ikiondoka na shilingi 1,004,618 na uwanja
ukipata shilingi 4,305,508.
Aidha, baadhi ya viongozi wa timu za
Tanzania Prisons na Mbeya City ambao hawakutaka kutajwa majina yao wameutaka
uongozi wa uwanja wa Sokoine kudhibiti mianya ya wazi ambayo imetokana na
mashabiki kutoboa baadhi ya kuta na kuingia ndani ya uwanja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “JUMLA YA SHILINGI MILION 37,410,000 ZIMEPATIKANA KATIKA MECHI YA MBEYA CITY &TANZANIA PRISONS.”
Post a Comment