Thursday, March 20, 2014
KINGUNGE AKERWA NA SERIKALI 3.
Do you like this story?
MWANASIASA wa siku nyingi
muumini wa siasa ya ujamaa kingunge ngombale mwiru, amesema tume ya
mabadiliko ya katiba ya jaji
warioba imeangaliza zaidi kero za muungano katika kudai serikali tatu hali ambyao inavunja muungano.
Akizungumza katika
mahojiano maalumu alisema tume ilipaswa kuangalia changamoto zilizopo ili zirekebishwe na kuimarisha
muugnano lakini si kushauri kuvunja kwa kuunda serikali tatu.
Tume ingeenda na kazi ya
kujenga na sasa inabomoa kwani wamekuwa wakitazama zaidi kasoro baada ya kuona
kuna kero kwenye muungano wangeleta marekebisho na kufanya kazi ya kuleta
mapendekezo alisema.
Amesema kuruhusu serikali
tatu tutakuwa na nchi ya ajabu hilo limefanyika wapi duniani? Serikali tatu
kwenye nchi moja akaohoji kingunge.
Amesema marekani wana
serikali zaidi ya 50 na wamekuwa wazalendo
kwenye nchi yao na hakuna wa kuwagusa hata china na indiaa wako vivyo
hivyo.
Amesema suala la kuwa na
katiba mpya kuna haja ya kutafakari na
kuona cha kufanya na kuhakikisha inapatikana kativa bora zaidi kuliko iliyopo sasa na bila hivyo hakuna sababu ya
kupata katiba mpya.
Pamoja na hayo amesema
tume ya marekebisho ya katiba haikuheshimu
wananchi na mapendekezo katika
sura ya kwzna juu ya kuungano wa Tanzania kwani mapendekezo yao ni kuundwa kwa shirikisho .
Amesema rasimu hiyo
haizungumzii jamhuri ya muungano wa Tanzania iliyopo leo na uhalali wake baada ya kuundwa kwa
shirikisho la nchi mbili.
Aidha amesema ili kupata
shirikisho wanaounda shirikisho wanaanza na ushirika.
Tatizo la wenzetu wa tume
wanafanya kazi ya kuuliza wananchi na
wameangalia zaidi kero kwenye suala la muungano lakini kero ziko katika aina
zote za serikali hata serikali za shirikisho zina kero zake amesema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KINGUNGE AKERWA NA SERIKALI 3.”
Post a Comment