Thursday, March 20, 2014
MICROSOFT YAJA NA JIBU LA TATIZO LA WIZI MITANDAONI.
Do you like this story?
Kampuni ya Microsoft
inayojishughulisha na utengenezaji wa kompyuta pamoja na proframu imebuni mbinu
mpya ya kukabiliana na wizi wa
mitandaoni ambao umezisababishia hasara benki, kampuni na watu binafsi katika maeneo mengi duniani.
Mkakati huo umekuja wakati
benki nyingi nchini zikiathiriwa na wizi huo kupitia mashinde za kutolea
fedsha maarufu kama ATM pamoja na miamala
inayofanyka kupita mifumo ya mawasiliano
ya kompyuta.
Takwimu zinaonyesha katika
kipindi cha oktoba 2012 hadi februari
2013 tanzania inakadiriwa kuwa n ash 700
milioni ziliibiwa katika benki kwa nyakati tofauti.
Kutokana na halihiyo
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania Profesa Benno Ndulu aliziagiza taasisi za
fedha kuchukua hatua ili kukabiliana na
hali hiyo.
Taarifa kwa vyambo vya
habari iliyotolewa na mkurugenzi mkuu wa
kampuni ya Microsoft , David Finn
imeeleza kuwa wamebuni kompyuta
mpya pamoja na program ambazo zinaziba mianya ya wizi.
Imeweka wazi kuwa uuzaji
holela wa program za kompyuta duniani umekuwa chanzo cha wezi hao kutumia
ujanja huo katika kufahamu taarifa za siri zilizohifadhiwa kwenye kompyuta za taasisi zn hata watu binafsi zilizounganishwa kwenye mtandao.
Utafiti ulitolewa mwka huu
na kampuni ya kimtaifa ya teknolojia ya mawasiliano ya kompyuta ikishirikiana na chuo kikuu cha Singapore
unayonyesha wizi wa kwenye mtandao
unaogharimu kampuni zaidi ya dola za kimarekani
billion 315 kwa mwaka sawa na sh 504 trilioni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MICROSOFT YAJA NA JIBU LA TATIZO LA WIZI MITANDAONI.”
Post a Comment