Sunday, March 30, 2014
KUTOKAMILIKA KWA MIRADI MINGI KWA WAKATI JIJINI MBEYA WADAU WATOA USHAURI.
Do you like this story?
Soko jipya la Mwanjelwa jijini Mbeya
ambalo ujenzi wake umekuwa wa kusuasua
|
![]() |
Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Dkt.Samweli Razaro, akifafanua kero mbalimbali za wafanyabiashara jijini Mbeya |
![]() |
Wafanyabiashara mbalimbali wa jiji la mbeya wakiwa katika ukumbi wa Mkapa uliopo maeneo ya Soko matola. |
HALMASHAURI
ya Jiji la Mbeya, imeshauriwa kupunguza posho za madiwani wakati wa vikao vya
baraza kutokana na kushindwa kupitisha miradi ya maendeleo inayotekelezeka kwa
wakati.
Ushauri huo,
umetolewa jijini Mbeya na wafanyabiashara wa Jiji la Mbeya kwenye
mkutano na uongozi wa halmashauri uliokuwa ukijadili changamoto
mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo ya ongezeko kodi.
Wamesema,
miradi mingi ya maendeleo inayopitishwa na baraza hilo imeshindwa kutekelezeka
kwa wakati hivyo ni vema uongozi wa halmashauri ukawapunguzia kiwango cha
posho wahusika ili kiendane na kipimo cha uwajibikaji.
.
Kwa upande
wake, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Dkt.Samweli Razaro, ambaye licha ya
kuahidi kulichukua suala hilo na kulifikisha kwenye mamlaka husika lakini
alitumia nafasi hiyo kuwafafanulia wafanyabiashara sababu zilizosababisha
kushindwa kukamilika kwa wakati ujenzi wa soko la Mwanjelwa.
Amesema,
awali ujenzi huo ulikuwa chini ya mkandarasi kutoka Kampuni ya Tanzania Bulding
Works Limitted ya Jijini Dar es Salaam ambaye alikiuka makubaliano ya mkataba
hivyo halmashauri kuvunja na kuingia mkataba mpya na
mkandarasi kutoka Kampuni ya Nandhra Engineering & Construction
Company.
Hata
hivyo,Dkt, Razaro alisema kuwa mkandarasi huyo mpya anatarajia
kutumia shilingi bilioni 5.0 katika kukamilisha ujenzi wa soko hilo na
kukabidhi kwa uongozi wa halmashauri ifikapo mwezi Desember mwaka huu.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KUTOKAMILIKA KWA MIRADI MINGI KWA WAKATI JIJINI MBEYA WADAU WATOA USHAURI.”
Post a Comment