Wednesday, March 19, 2014
RAIS ZUMA” ALIFYOZA PESA ZA UMMA.
Do you like this story?
Ilivyokuwa nyumba ya Zuma kabla ya kukarabatiwa |
Nyumba ya Zuma Baada ya kukarabatiwa |
Ripoti iliyosubiriwa kwa hamu kuhusu
ufisadi nchini Afrika Kusini, imemkosoa vikali Rais Jacob Zuma kwa kujinufaisha
na pesa zilizotumiwa kuikarabati nyumba yake binfasi katika mkoa wa Kwazulu
Natal.
Ukarabati huo uligharibu dola
milioni 23.
Katika ripoti yake , mdhibiti wa
mali ya umma nchini humo,Thuli Madonsela, amesema kuwa Zuma alikiuka sheria za
maadili na kujifaidisha na pesa za Umma.
Inaarifiwa Zuma alisisitiza
ukarabati huo, ufanywe.
Hata hivyo, ripoti hiyo ilisema kuwa
hakudanganya wabunge kuhusu kashfa hiyo. Kadhalika wito umetolewa kuwa Zuma
arejeshe sehemu ya pesa hizo ambazo hazikutumika kwa ajili ya usalama wake au
vinginevyo.
Vyombo vya habari nchini humo
vinadai kuwa baadhi ya pesa za umma zilitumiwa katika kufadhili mahitaji ya
kifahari ya bwana Zuma kama bwawa la kuogelea na chumba cha sinema.
Mwandishi wa BBC nchini humo anasema
kuwa ripoti hiyo itaathiri pakubwa sifa ya Zuma na chama tawala ANC, huku
akijiandaa kwa uchaguzi mkuu katika kipindi cha wiki sita.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RAIS ZUMA” ALIFYOZA PESA ZA UMMA.”
Post a Comment