Friday, March 14, 2014

SITTA: KURA Y A SIRI.




Mwenyekiti mteule wa Bunge maalumu  la katiba Samuel sitta amezungumzia uwezekano wa kutumia kura ya sira katika  kuamua  idara nyeti  katika rasimu ya katiba.

Sitta aliyechaguliwa juzi kuhika wadhifa huo alisema atashirikiana na kamati ya uongozi  itakyoundwa  ya wenyeviti  wa kamati 15 za bunge hilo na kamati ya ushirikiano  kupata jawabu la suala hilo.

Akizingumza katika mahojiano maalumu  nyumbani kwake  mjini Dodoma juzi, sitta alisema: unajua kuna baadhi ya vifungu na ibara za rasimu ya katiba ni vizuri  vipigiwe  kura ya wazi na vingine ambavyo ni nyeti  zaidi vipigiwe kura ya siri”

Amesema si vizuri  vifungu  vyote vipigiwe kura sawa  yaani si lazima zote ziwe za siri au ziwe za wazi.

Alitoa mfano wa ibara inayosema kutakuwa na mahakama kuu ya Tanzania na kusema: “Hatuwezi kushindana katika suala la kuwapo kwa mahakama ni ni wazi kuwa jambo hilo mnaweza  kupiga kura ya wazi nasema hivyo kwa sababu kativa yoyote lazima ionyesha mihimili yote ambayo bunge, serikali  na Mahakama.

Sitta ambaye pia ni waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki alishinda kiti hicho katika uchaguzi uliofanyika  juzi kwa kura 487  kati ya 563(sawa sawa na asilimia 85)

Mbunge huyo wa urambo  mashriki ambaye kaulimbiu  yake ni kasi na viwango alisema vifungu na ibara za rasimu ya katiba vinavyoweka misingi ya kativa ni vizuri vikapigiwa kura ya siri.

Unajua tuna viongozi wa dini na halitakuwa jambo  la busara kama tukizijua hisia zao. Kama wewe uko karivu na imamu au askofu halafu anapiga kura ya wazi ya kutaka serikali tatu wkati wewe muunini unataka serikali mbili ni wazi kuwa jambo hilo linaweza kuleta hisia tofauti na kuwanyima watu haki na uhuru wa kuamua alisema sitta.

Alitoa mfano wa sura ya sita ya rasimu ya katiba inayozungumzia  serikali na muundo  wa madaraka katika jamhuri  ya mungano na kufafanua  kuwa katika sura hiyo atapendekeza ipigiwe kura ya siri.

Kuhusu suala hilo la muundo wa serikali alisema  kikubwa ni wajumbe kujenga hoja hatuwezi kwenda na msimamo isiyobadilika kwa sababu tunataka maridhiano . nitatenda haki  na nitatoa muda mrefu zaidi kwa wajumbe kujadili sura ya kwanza nay a sita ambazo zina uzito  mkubwa kuliko sura nyingine ambazo ni za maelezo tu. Mano suala la haki za binadamu ambazo wote tunakubaliana nazo.

Amesema wakati wa kujadili moundo huo wa serikali ndani ya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ukifika ataishauri kamati ya uongozi  kutenga muda wa ziada katika suala hilo na  mengine yenye utata.

Mwenyekiti huyo alisema suala la upigaji kura linatakiwa kuamuliwa kwa busara na atatumia hekima zake na za wajumbe wa bunge hilo kutatua mgogoro wa kura ya siri au ya wazi.


0 Responses to “SITTA: KURA Y A SIRI.”

Post a Comment

More to Read