Friday, March 21, 2014
THAMANI YA TAUSI WAIJUA POLISI PAKISTAN.
Do you like this story?
Tausi wa Pakistan |
Polisi watatu wanaolinda makazi
ya waziri mkuu wa Pakistan wamesimamishwa kazi kwa muda baada ya Paka kumuua
Tausi wa waziri mkuu.
Mtunza bustani alipata Tausi mmoja amekufa katika
moja ya bustani za makazi ambapo ndege hao huvinjari , lilieleza gazeti la
Express Tribune.
Mmoja wa maafisa waliosimamishwa kazi amesema
wengine 21 waliitwa kujieleza baadae. Imeripotiwa kuwa maafisa hao walisema
walikuwa kazini usiku ule , lakini hawakutegemea kuwa Paka wangemla Tausi.
Maafisa 18 hawakubainika kuwa na hatia,
gazeti lilieleza.
Lakini watatu waliosalia wote walipewa onyo
na kuadhibiwa kwa uzembe
Makazi ya waziri mkuu wa Pakistani Nawaz
Sharif yako Raiwind, viungani mwa mji wa Lahore.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “THAMANI YA TAUSI WAIJUA POLISI PAKISTAN.”
Post a Comment