Friday, March 28, 2014
WILAYA YA MAKETE YATAJWA KUWA MIONGONI MWA WILAYA 41 ZITAKAZOPEWA FEDHA KWA AJILI YA UJENZI WA NYUMBA BORA ZA WAALIMU
Do you like this story?
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete amewaambia Wananchi wa Tanga, jana tarehe 27 Machi,2014 wakati
akihutubia Mkutano wa hadhara katika barabara ya Karume kuwa;
"Tayari
Halmashauri za Mkinga, Pangani na Kilindi zimeshapata pesa hizo , na tumetenga
kiasi kama hicho kwa kila Halmashauri zingine nchini ili kuboresha makazi
na Nyumba za Walimu " Rais amesema.
Fedha hizo ni
sehemu ya fedha iliyotengwa maalum na Serikali kwa ajili ya kujenga nyumba za
walimu katika Halmashauri arobaini na moja (41) nchini kote katika
kipindi cha Mwaka wa fedha wa 2013/14.
Halmashauri zingine zitakazofaidika na mpango huo ni Mlele, Nsimbo ,
Meatu, Makete, Ngorongoro na Longido. Pia Halmashauri za Bagamoyo, Mafia,
Kisarawe, Rufiji,, Kigoma, Kasulu, Kibondo, Nachingwea, Kilwa, Liwale,Ruangwa
Rorya, Chunya, Ileje, Rungwe, Kilombero, Ulanga, Newala, Tandahimba na
Nanyumbu zitafaidika na mpango huo wa Serikali.
Aidha,
Halmashauri za Ukerewe, Sengerema, Kwimba, Tunduru, Namtumbo na Sikonge pia
zimo katika mpango huo wa Mwaka huu wa fedha.
Halmashauri za Muleba, Ngara, Nkasi, Kiteto na Simanjiro nazo zimo katika
mpango huu ambao Serikali imedhamiria kuutekeleza ili hatimaye
kuwatengenezea mazingira mazuri walimu hapa nchini.
Rais amemaliza awamu ya kwanza ya ziara yake ya kikazi Mkoani Tanga
ambapo ametembelea, kukagua shughuli za maendeleo na kufungua miradi ya
Barabara, Maji, Soko na Maabara Mkoani Tanga.
Katika ziara yake hiyo Rais ametembelea Wilaya za Handeni, Korogwe,
Muheza na Tanga ambapo katika awamu ya pili Rais amepanga kutembelea Mkinga,
Lushoto, Kilindi na Pangani.
Rais amerejea jijini Dar es Salaam jana jioni.
Imetolewa na;
Premi Kibanga
Mwandishi wa Habari
wa Rais Msaidizi,
Tanga.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WILAYA YA MAKETE YATAJWA KUWA MIONGONI MWA WILAYA 41 ZITAKAZOPEWA FEDHA KWA AJILI YA UJENZI WA NYUMBA BORA ZA WAALIMU”
Post a Comment