Saturday, May 24, 2014

BAADA YA KUTEMWA KIKOSI CHA BRAZIL, RONALDINHO AAMUA KUPANGISHA NYUMBA YAKE YA RIO de JANEIRO, KODI HIYO mhhhhh!






BAADA ya kuachwa katika kikosi cha Luiz Felipe Scolari kitakachoshiriki kombe la dunia  katika ardhi ya nyumbani, Ronaldinho `Gaucho` amebuni njia mpya ya kuingiza mkwanja kwenye mashindano ya kombe la dunia yanayoanza majira ya kiangazi mwaka huu.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Barcelona ameamua kupangisha nyumba yake iliyopo mjini Rio de Janeiro kwa kodi ya Euro 9, 120 kwa usiku mmoja, lengo likiwa ni kuwapa mashabiki fursa ya kula bata kwenye mjengo wa gwiji huyo wa Brazil.

Ronaldinho aliandika katika mtandao wake wa Twita kuthibitisha kuwa nyumba yake yenye vyemba vitano ipo tayari kwa ajili ya kupangishwa wakati wa mashindano na kama mtu anahitaji anatakiwa kufanya `mambo` kupitia tovuti ya Airbnb.com.

0 Responses to “BAADA YA KUTEMWA KIKOSI CHA BRAZIL, RONALDINHO AAMUA KUPANGISHA NYUMBA YAKE YA RIO de JANEIRO, KODI HIYO mhhhhh!”

Post a Comment

More to Read