Tuesday, May 20, 2014
BUNGE LAINGILIA KATI SUALA LA UDA
Do you like this story?
Dar es
Salaam. Wakati mjadala kuhusu umiliki wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA)
ukiendelea kuwa tata, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imemwita
Msajili wa Hazina na mwendeshaji wa shirika hilo ili kujadili suala hilo na
kumaliza mgogoro wake.
Mwenyekiti
wa PAC, Zitto Kabwe alisema jana kuwa hatua hiyo itamaliza suala hilo ambalo
limezua malumbano bungeni baina ya Serikali na baadhi ya wabunge juu ya umikili
wa kampuni hiyo.
Mgogoro
wa umiliki wa shirika hilo uliibuka wiki iliyopita bungeni na Naibu Waziri wa
Fedha, Adam Malima alisema bado linamilikiwa na Serikali kwa asilimia 49 na Halmashauri
ya Jiji la Dar es Salaam asilimia 51, wakati Kampuni ya Simon Group ikisema
ilishanunua asilimia 76 ya hisa za shirika hilo.
Wakati
mgogoro huo ukiwa haujafikia mwisho, UDA imetangaza kuagiza mabasi 2,000
yanayotarajiwa kuingia nchini Agosti mwaka huu kwa ajili ya kuboresha huduma ya
usafiri huo.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena amesema,
“Tuna mkakati wa kununua mabasi 2,000 mwaka huu ambayo tayari tumeshayaagiza na
mpaka Agosti yatakuwa yameingia. Mpaka sasa tunayo mabasi 300 yanayofanya kazi
huku mengine 200 yakiwa bado yapo ‘yard’ yakisubiri kukamilika kwa taratibu za
kuyatoa,” alisema Kisena.
Mabasi
hayo mapya yatagharimu Sh300 bilioni na kuinua uwezo wa shirika hilo
kusafirisha abiria wengi zaidi ukilinganisha na hali ilivyo sasa, huku uongozi
ukijipanga kushughulikia changamoto zilizopo.
Mkurugenzi
huyo aliyesisitiza kuwa anamiliki kihalali shirika hilo, aliongeza kuwa
mchakato wa kusajili shirika hilo katika Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE)
unaendelea.
Akizungumza
juu ya utata uliojitokeza bungeni kuhusu uhalali wa kampuni yake kuendesha na
kusimamia shughuli za shirika hilo, Kisena alisema kuwa anafanya hayo yote kama
mkataba unavyosema na akawashangaa wabunge wanaoonyesha kutofahamu
kinachoendelea.
Kisena
aliongeza kuwa katika vikao vya wanahisa na hata vile vya uongozi wa jiji vya
kuiuzia kampuni yake hisa za UDA, wabunge walikuwapo na walikubaliana na ajenda
zilizofikiwa kabla ya utekelezaji wake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ BUNGE LAINGILIA KATI SUALA LA UDA”
Post a Comment