Sunday, October 26, 2014
MOI YATOA TAARIFA, YADAI BODABODA HUUMIZA VICHWA VYA WATU 600 KILA MWEZI
Do you like this story?
TAASISI ya Tiba ya
Mifupa Muhimbili( MOI), imesema kwa mwezi inapokea wagonjwa 600 walioumia
vichwa kutokana na ajali za Pikipiki.
Akizungumza na
Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa taasisi hiyo,
Patrick Mvungi, alisema ajali hizo zinasababishwa na madereva pamoja na abiria
kushindwa kuvaa kofia ngumu pindi wanapokuwa barabarani.
Mvungi, alisema
taasisi hiyo ikiwa katika kipindi cha mpito cha mageuzi ya utoaji huduma za afya
nchini, imefanikiwa kwa asilimia 95 kutoa huduma muhimu za tiba na upasuaji kwa
wagonjwa na hivyo kupunguza vifo na rufaa za kusafirisha wagonjwa nje ya nchi.
Alisema zaidi ya
wagonjwa 4,500 wa mifupa wamepatiwa huduma kwa kutumia utaalamu wa kufanyiwa
upasuaji na kuwekewa kifaa maalum (Sign Nail), kwa wagonjwa waliovunjika mifupa
kinachowasaidia kupona mapema na kurudi katika hali zao za kawaida.
“Kwa upande wa
Upasuaji Mkubwa wa Nyonga (Total Hip Replacement), zaidi ya wagonjwa 1,256
walipasuliwa salama na wamepona, huku zaidi ya wagonjwa 703 wakifanyiwa
upasuaji mkubwa wa kubadilisha viungo vya goti vilivyoharibika (Total Knee
Replacement), kwa kuweka vifaa maalum vya bandia (Artificial
Implants), ambapo zaidi ya 95 ya wagonjwa wameweza kutembea na kurudi katika
hali zao za kawaida,” alisema.
Mvungi, alisema
taasisi hiyo pia imefanikiwa kutoa matibabu kwa wagonjwa ya ubongo (Brain
Surger diseases), waliokuwa wakihitaji upasuaji kwa zaidi ya asilimia 80.
Na Janeth Jovin
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ MOI YATOA TAARIFA, YADAI BODABODA HUUMIZA VICHWA VYA WATU 600 KILA MWEZI ”
Post a Comment